Thursday 4 December 2014

DAMU NZITO..BAADA YA MIAKA 35 BABA WA ROSE NDAUKA AJITOKEZA..




Mwanaume mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Severin Daniel Ndauka amejitokeza katika Ofisi za Global Publishers na kudai kwamba, staa wa sinema za Bongo, Rose Donatus Ndauka ni mtoto wa kaka yake ambaye alichukuliwa kutoka Tanga na kupelekwa jijini Dar.
Mzee huyo aliyekuwa akizungumza kwa kujiamini mbele ya waandishi wetu, alisema mwaka 1979, shemeji yake, Nyazimbili au mama Godwin (anayedaiwa ni mama wa Rose) alijifungua mtoto wa kike katika Kijiji cha Sakura wilayani Pangani, Tanga ambapo kwa bahati mbaya mama huyo alifariki dunia hivyo mtoto kuchukuliwa na kanisa ambalo lipo Msimbazi Dar hakutaka kulitaja jina lililomlea mtoto huyo kwa kuwa familia haikuwa na uwezo.
Mzee Severin Daniel Ndauka anaedai kuwa Rose Ndauaka ni mwanaye.
“Baada ya hapo, hatupata taarifa tena lakini mimi niliamua kuja Dar kwa ajili ya kumtafuta Rose. Nilikwenda Msimbazi, nilipofika nikaambiwa Rose alichukuliwa na kituo cha kulea watoto kilichopo Kurasini. Ilibidi niende Kurasini, kufika nikaambiwa alichukuliwa na msamaria mwema kwa ajili ya kumlea kama mtoto wake.

“Tangu hapo hatukupata taarifa nyingine lakini baadaye dada yangu anaitwa Maria Ndauka akanipigia simu, akasema amemuona Rose kwenye televisheni akiigiza na marehemu Steven Kanumba ndiyo nimekuja hapa mnisaidie kumpata,” alisema mzee huyo.
Rose alipotafutwa na kuelezwa ishu hiyo, alisema alizaliwa jijini Dar na si mwaka 79 kama alivyodai mtu huyo na kwamba katika  Kijiji cha Sakura hana ndugu.
Kama kuna Rose Ndauka mwingine, afike Ofisi za Global Publishers zilizopo Bamaga, Mwenge jijini Dar ili akutanishwe na mzee huyo.
SOURCE: GPL

No comments: