Saturday 29 November 2014

MAAJABU; JOKA LATOA PESA KUPITIA ATM...

SAKATA LA ESCROW,HATIMAYE WASIRA ATOA MATAMKO MAKALI..


JWTZ WAMPA KIPIGO BIBI WA MIAKA 60 HUKO KIGOMA


Bi.Mariam Abdallah

HELIKOPTA YAANGUKA JIJINI DAR NA KUUA WATANO


BARUA YA WAZI KWA WEMA SEPETU


HAMISA MOBETO ADAI HATEGEMEI WANAUME ILI AISHI MJINI



Hamisa Hassan Mobeto

HATIMAYE RAIS KIKWETE ATAJWA KUHUSIKA SAKATA LA ESCROW...SOMA UHUSIKA WAKE HAPA CHINI


HUYU NDIE VIDEO MODO MWENYE HIPS KUBWA KULIKO MAVIDEO MODO WOOOOOOOTE HAPA AFRIKA...



MAASKOFU WAKIRI KUPOKEA FEDHA ZA ESCROW....


               Baba askofu Methodius Kilaini.

 Askofu 
Msaidizi wa Jimbo la Bukoba, Methodius Kilaini amekiri kupokea Sh80.5 milioni kutoka kwa Mkurugenzi wa VIP Engeering, James Rugemalira akisema si mara yake kwa kwanza kupokea fedha kutoka kwa mfanyabiashara huyo kwa kuwa mara nyingi huwa anachangia kwa uwazi miradi ya jamii. 

MJADALA MZIMA WA SAKATA LA ESCROW NA MAAZIMIO YALIYOFIKIWA KATIKA VIKAO VYA JANA MCHANA NA JIONI..


MJADALA

Nchambi: Anailaumu serikali kwa kuchelewesha kuleta jambo husika bungeni, watanzania wana hamu ya kujua fedha ni nani? Wakili wa TANESCO(Mkono) alishauri kufunguliwa akaunti(ananukuu maandiko ya biblia kuhusu kuheshimu mamlaka), anasema kila mtu atawajibika kwa namna yake.

Friday 28 November 2014

MH.KANGI LUGOLA AVAA KININJA BUNGENI ILI ASIWATAZAME WAHUSIKA WA SAKATA LA ESCROW

HUYU NDIO DEMU MREMBO KULIKO WOOOOOOOTE DUNIANI KWA WAKATI HUU.......CHEKI MAFOTO YAKE


                                    Mwanamke Mzuri Kuliko Wote Duniani Kwa Mwaka 2013

Huyu sio mwingine bali ni Malkia wa Saudi Arabian, aitwae Fatima Zohar-Godabari.

Fathima Kulsum Zohar Godabari ambaye awali alikuwa kwenye familia ya kifalme kwa sasa yeye ndie Malkia wa Saudi Arabia.
Hivi karibuni alipigwa picha bila kuwa amevaa niqab ikiwa imefunika uso wake, na picha hizo kuchapishwa kisha kusambazwa kwenye mitandao, zikionyesha uzuri wa sura yake duniani ikiwa ni mara ya kwanza.

Toka picha hizo zitoke, watu wengi wamekuwa wakimtaja kuwa ndiye mwanamke mzuri duniani kwa sasa.
Cheki picha zake hizi hapa chini lazima utakubali.......

DIAMOND NA ZALI WAUMBUKAAAAAAA.....


Nasibu Abdul ‘Diamond’ na Zarinah Hassan wakibusiana kimahaba.
Licha ya madai wanayoyatoa mastaa wawili hot kwa sasa, Nasibu Abdul ‘Diamond’ na Zarinah Hassan a.k.a Zari au The Boss Lady kuwa si wapenzi bali kuna project wanaifanya, wawili hao wameumbuka.

MAGAZETI YA KIBONGO YA LEO

MAGAZETI YA MICHEZO NA UDAKU LEO HII

UNICEF KUJENGA MAHAKAMA YA WATOTO MKOANI MBEYA


Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia watoto Duniani UNICEF limeahidi kusaidia ujenzi wa Mahakama ya watoto Mbeya kutokana na Mkoa huo kukidhi viwango vya uanzishwaji wa Mahakama hiyo ambapo hii itakuwa ni Mahakama ya pili kwa Tanzania, nyingine ikiwa ni Mahakama ya Kisutu Dar.

VIONGOZI WA AFRIKA WAASWA KUACHA KUNG'ANG'ANIA MADARAKA


Raisi wa Ufaransa Francois Hollande amewapa somo viongozi wa bara la Afrika,kwamba wanapaswa kujifunza kwa yale yaliyotokea nchini Burkinafaso na sio kung'ang'ania madarakani.

Kauli ya raisi Hollande imetoka katika mkutano wa nchi zinazozungumza kifaransa ,unaofanyika nchini Senegal,na kutolea mfano kwa kile kilichomkuta na kumuondoa madarakani Blaise Compaore na kutilia mkazo suala la katiba kuheshimiwa.

NCHI NYINGI ZA AFRICA KUTOFIKIA MALENGO YA MILLENIA


Nchi nyingi za bara la Afrika hazitaweza kufikia malengo ya milinia ifikapo mwaka 2015 kutokana na mwanya uliopo kati ya uchumi na maendeleo ya kibinadamu. Haya ni kwa mujibu wa ripoti ya kila mwaka ya Umoja wa Mataifa juu ya nchi zenye maendeleo madogo, iliyowasilishwa Alhamisi.

Licha ya kukua kwa uchumi barani Afrika nchi nyingi hazitafikia malengo ya milinia (MDGS) mwakani. Afisa wa maswala ya kiuchumi kwa Afrika katika Umoja wa Mataifa Junior Davis anasema nchi nyingi za Afrika  hazijaweza  kutumia maendeleo ya kiuchumi kufanya mabadiliko  katika sekta zake za miundo mbinu.

WAZIRI Prof MUHONGO ASEMA FEDHA ZA ESCROW SI MALI YA UMMA,ADAI BADO SERIKALISERIKALI INADAIWA..



Akiwasilisha maelezo ya Serikali leo, Prof Muhongo alipangua hoja moja baada ya nyingine zilizotolewa na Kamati ya PAC jana na kusisitiza kuwa fedha hizo si mali ya umma.

Sakata la uchotwaji wa fedha katika Akaunti ya Tegeta Escrow linaendelea kuchukua sura mpya baada ya Waziri wa Nishati na Madini, Prof Sospeter Muhongo kutoa ufafanuzi wa Serikali bungeni mjini Dodoma kuwa fedha hizo si za umma na kwamba bado Serikali ina mzigo wa madeni katika sakata hilo.

Kauli ya Prof Muhongo inakuja siku moja baada ya Kamati ya PAC kuwasilisha ripoti yake jana juu ya suala hilo ambapo pamoja na mambo mengine, Kamati ya PAC ilijiridhisha kuwa sehemu ya fedha hizo ni za Serikali.

Mwenyekiti wa PAC, Zitto Kabwe akisoma taarifa ya kamati hiyo jana alisema Kaimu Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Francis Mwakapalila, Kamishna Mkuu wa TRA, Rished Bade wakithibitisha kuwa sehemu ya fedha zilizokuwamo kwenye Akaunti ya Tegeta Escrow zilikuwa za Serikali.

Akiwasilisha maelezo ya Serikali leo, Prof Muhongo alipangua hoja moja baada ya nyingine zilizotolewa na Kamati ya PAC jana na kusisitiza kuwa fedha hizo si mali ya umma.

Prof Muhongo pia alitumia muda mwingi kueleza jinsi Kampuni ya uwakili ya Mkono and Advocates iliyokuwa ikiitetea Serikali pamoja na Tanesco, ilivyochota kiasi kikubwa cha pesa kama malipo ya kazi hiyo tangu kuanza kwa mgogoro huo.

“Gharama za mawakili; Kampuni ya Mkono & Advocates waliokuwa wakiitetea Tanesco na Serikali katika suala la IPTL tangu mwaka 1998 hadi 2013 ni Sh62.90 bilioni na bado wanaidai Serikali $ milioni nne,” alismea Prof Muhongo.

Aliongeza kuwa Kampuni hiyo ya Mkono & Advocates iliishauri Serikali kuwapa kazi nyingine ya kwenda kuitetea Serikali juu ya mgogoro huo, lakini Serikali ilikataa na kuongeza kuwa waliokoa Sh95 bilioni kwa uamuzi huo kwani uwezekano wa kushinda ulikuwa mdogo.

DIAMOND NDANI YA JUMBA LA BIG BROTHER AFRICA










Hii ni mara ya pili kwa msanii Diamond Platnumz kualikwa ndani ya jumba la BBA akiwa na mwanamuziki kutoka Congo, Fally Ipupa ambapo wameshiriki chakula cha mchana pamoja na washiriki waliobaki kwenye Jumba hilo, safari hii wasanii hao wameingia kwa ajili ya kuhamasisha ONE Campain ambayo inahusu kilimo, moja ya Project zilizowahi kufanywa na Kampeni hiyo ni ile nyimbo ya Cocoa na Chocolate ambayo wameshiriki pia mastaa wengine kibao kutoka Afrika.

KOCHA WA CHELSEA APEWA KAZI KUINOA GHANA


Mkufunzi wa zamani wa Chelsea Avram Grant ameteuliwa kuwa kocha mpya wa Ghana.

Kocha huyo mwenye umri wa miaka 59 alitia saini kandarasi ya kufunza kwa miezi 27 na kuchukua uongozi kutoka kwa Maxwell Konadu, ambaye amekuwa kocha wa muda tangu Kwesi Appiah alipoondoka mwezi wa Septemba.

Ataanza kazi Jumatatu na mkataba wake kumalizika mwishoni mwa Februari 2017 - baada ya fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika.

Raia huyo wa Israeli ana wiki sita tu kuiandaa Black Stars kwa ajili ya kombe la mataifa ya Afrika mwaka 2015 nchini Equatorial Guinea.

Shirikisho la kandanda nchini Ghana limetoa ruzuku kwake kwa "kufanya vizuri" katika mashindano hayo na amepewa muda mfupi na timu hiyo na kuwa atashinda kombe hilo miaka miwili ijayo.

Ghana, ambayo iliongoza katika kufuzu kwenye kundi lao ili kushiriki mashindana hayo mwaka ujao, itapata kujua wapinzani wao nchini Equatorial Guinea wakati droo itakapofanywa tarehe 3 Desemba.

Mashindano yatafanyika kati ya Januari 17 na 8 Februari.

Grant, ambaye alikuwa kocha mkuu wa timu ya Chelsea alishindwa na Manchester United katika fainali za mwaka wa 2008 katika Ligi ya Mabingwa, alipohudumu hadi hivi majuzi ambapo alichaguliwa kuwa mkurugenzi wa kiufundi katika klabu ya BEC Tero Sasana nchini Tahailand.

Jukumu lake la mwisho kama kocha lilikuwa katika klabu ya Partizan Belgrade kati ya mwaka 2012-2014, wakati ambapo aliongoza klabu hio kutwaa ubingwa wa ligi kwa mara ya tano.

Kando ya kuviongoza vilabu vya Uingereza vya Portsmouth na West Ham, Grant ana uzoefu wa kimataifa kwani aliifunza timu ya taifa ya Israeli kwa miaka minne.

Kumekuwa na wale wamekuwa na wasiwasi kwamba utaifa wa Grant ungeweza kumzuia kuingia baadhi ya nchi za Afrika Kaskazini.

Rais wa shirikisho la kandanda nchini Ghana, Kwesi Nyantekyie aliiambia BBC Michezo "kwamba ni suala" lakini anasema kuwa pande hizo mbili zitakabiliana nalo.

"Mmiliki wa pasipoti ya nchi ya Israel hatakataliwa tu kuingia nchi za Afrika Kaskazini,bali pia atazuiliwa kuingia baadhi ya nchi za Kiarabu," alisema.

"Yeye ameleta njia mbadala ya kukabiliana nayo. Kuna utaratibu wa kuridhisha wa kukabiliana na tishio lake.

Hivi karibuni, katika miezi michache ijayo, tutashughulikia kikamilifu mambo hayo."
CHANZO: BBC


BI HARUSI AMLISHA MUMEWE SUMU


Bi harusi wa miaka 14 nchini Nigeria ameshtakiwa kwa kuwaua watu wanne akiwemo mumewe wa miaka 35 baada ya kuweka sumu ya panya katika chakula alichoandaa kwa sherehe za haruysi yake.

Kesi hiyo imewashangaza wahaharakati wa haki za kibinaadamu ambao wamesema kuwa msichana aliyeozwa kwa mume aliye mara mbili umri wake anafaa kuchukuliwa kama mwathiriwa na wala sio muhalifu.

Wasila tasiu kutoka familia masikini katika eneo la waislamu la kazkazini huenda akakabiliwa na kifo iwapo atahukumiwa.

Shahidi wa kwanza wa kiongozi wa mashtaka Lamido Abba Sorron-Dinka alikuwa msichana wa miaka 7 anayejulikana kama hamziyya,ambaye alikuwa akiishi katika nyumba moja na Tasi'u pamoja na mumewe Umar sani,wakati bi haru huyo alipoweka sumu ya panya katika chakula hicho.

Hamziyya alijulikana tu kama dadaake mke wa kwanza wa bwana Sani,mwanamke aliyeolewa na marehemu awali katika eneo ambapo ndoa za wake wengi zimekithiri.

Msichana huyo wa miaka 7 alisema kwamba Tasi'u alimpa fedha ili kununua sumu ya panya kutoka duka moja jirani mnamo tarehe 5 mwezi Aprili,siku ambayo bwana Sani alifariki.

''Alisema kuwa panya wanamsumbua katika chumba chake'',Hamziyya aliiambia mahakama.Upande wa mashtaka baadaye ulisema kuwa badala yake Tas'u aliweka sumu hiyo ya panya katika chakula ambacho alikuwa amekiandaa kwa sherehe za baada ya harusi kwa kuwa alijuta uamuzi wake wa kumuoa bwana Sani.

Msichana huyo alikataa kuzungumza mahakamani.

Jaji Mohammed Yahaya,katika mahakama ya Gezawa alitoa hukumu kwamba Tasi'u ambaye alikataa kuongea katika mahakama hana hatia katika kusikizwa kwa kesi mnamo mwezi Octoba ambapo alisomewa mashtaka.

Jaji huyo alikataa ombi la upande wa mshtakiwa la kesi hiyo kupelekwa katika mahakama ya watoto.

Ushahidi wa Hamziyya uliungwa mkono na Abuwa Yussuf muuzaji duka katika mji wa Unguwar Yansoro ambaye alithibitisha kuuza sumu hiyo kwa mtoto huyo.

Jirani ya Bwana Sani mwenye umri wa miaka 30 ambaye ni mkulima, Abdulrahim Ibrahim alitoa ushahidi ambapo alisema kwamba alipewa chakula hicho kilichopikwa na Tasiu.''Nilipoletewa chakula hicho niliona vipande vipande vyeusi''aliiambia mahakama.

Alikula vipande vinne vya madonge vilivyotengezwa na maharagwe lakini hakupendelea ladha yake'',alisema na kuongezea kuwa ni Umar pekee aliyeendelea kula.

Baadaye alisema kuwa alimuona bwana Sani katika bustani ,akiwa mgonjwa na kumpeleka nyumbani.

Lakini alipokuwa akijaribu kumuuguza bwana sani ,aligundua kwamba watu wengine watatu ambao walikuwa wamekula chakula hicho wamefariki kwa ghafla.

Viongozi wa mashtaka walidai kwamba chakula cha Tasiu kilichowekwa sumu kiliwaua watu wanne na hivyobasi kuwajumuisha wanne hao katika kesi moja ya mauaji.

Nigeria haijawahi kumyonga mtoto aliyefanya uhalifu tangu mwaka 1997,ambapo taifa hilo liliongozwa na dikteta Sani Abacha,kulingana na shirika la kibinaadamu la Human Rights Watch.
CHANZO: BBC

SHEIKH PONDA AACHIWA HURU NA MAHAKAMA KUU


Mahakama Kuu ya Tanzania imemuachia huru aliyekuwa Katibu wa Taasisi za Kiislam, Sheikh Ponda Issa Ponda baada ya kuona hana hatia dhidi ya Kesi ya madai ya Ardhi ya Agrekanza inayomilikiwa na Afidhi Self  iliyokuwa inamkabili.

Akisoma Mashtaka hayo Mwanasheria wa Serikali, Tumaini Kweka mbele ya Jaji, Augustino Shangwe alisema baada ya kupitia vifungu vyote mahakama imejiridhisha na kuona Sheikh Ponda hana hatia yoyote na kumuachia huru tangu leo lakini katika hali ya kushangaza Sheikh Ponda amerudishwa rumande akisubiri kesi nyingine ya madai ya uchochezi,  Mkoani Morogoro inayomkabili.

Thursday 27 November 2014

MAITI ZA WALIOKUFA KWA EBOLA ZATUPWA HOVYO MTAANI


Wahudumu wa Afya nchini Sierra Leone waliopewa kazi ya kuzika maiti za wagonjwa waliokufa kwa ebola wameamua kuitupa miili hiyo mitaani kutokana na kulalamikia posho ndogo wanazolipwa na Serikali ya nchi hiyo.
Katika kitendo cha kushangaza waliamua kutupa miili 15 ya maiti hizo katika mitaa mbalimbali kwa lengo la kuelezea hisia zao za kuchoshwa na malipo madogo wakati wanafanya kazi kubwa.
Wafanyakazi hao waliripotiwa kukaa siku saba bila kulipwa fedha zao ambapo kwa wiki hulipwa dola100 ambazo walidai ni ndogo ukilinganisha na kazi waliyokua wakifanya kudai inahatarisha maisha yao kwa kiasi kikubwa.
Nyongeza ya fedha hizo walizokua wakitaka ni kwa ajili ya kufidia kazi wanazofanya kwa sababu hufanya katika mazingira magumu ya kuzika wagonjwa wa Ebola ambao huambikizwa kwa njia ya kugusana.
Kituo cha kitaifa kinachosimamia ugonjwa wa Ebola nchini humo kilitangaza rasmi kuwa wafanyakazi wote walioshiriki katika mgomo huo watafukuzwa kazi.

EMERSON AANZA MAZOEZI YANGA


Emerson de Oliveira Neves Roque  – mbrazil ambaye ameletwa nchini kuja kufanya majaribio na endapo ikifuzu basi ndio itachukua nafasi ya mbrazil aliyeondoka Jaja.Jana jioni mchezaji huyo huyo aliwasili na leo hii mchezaji huyo ameanza mazoezi mepesi asubuhi katika Uwanja wa shule ya Sekondari Loyola kufuatia kusaifri kwa zaidi ya masaa 11 kutoka jijini Rio de Janeiro.

Kiungo mbarazil Emerson de Oliveira a(wa pili kutoka kulia) akiwa mazoezini leo asubuhi katika uwnaja wa shule ya sekondari Loyola, wengine ni Kizza, Javu na Coutinho
Emerson ameungana na wachezaji wengine wa Young Africans katika mazoezi ya leo asubuhi ikiwa ni siku yake ya kwanza katika ardhi ya Tanzania na kufanya mazoezi mepesi mepesi chini ya kocha msaidizi Leonardo Neiva kuijiweka fit na kutoa uchovu safari.
Kiungo huyo mwenye umbo lililonyumbulika ambae alikuwa akichezea timu ya Bonsucesso FC iliyopo lii daraja la pili nchini Brazi katika jiji la Rio de Janeiro pia msimu uliopita alikua akicheza soka la kulipwa katika nchi ya Poland latika klabu ya Piotrkow Trybunalski FC.
Kocha mkuu wa Young Africans Marcio Maximo amesema mchezaji huyo leo alikua na programu ya mazoezi mepesi tu kutokana na uchovu wa safari na kesho anatarajiwa kuendelea na mazoezi na wenzake kulingana na ratiba iliyopo.
Endapo Emerson atafanikiwa kulishawishi benchi la Ufundi kumsajili  basi moja kwa moja ataingia makubaliano na klabu ya Young Africans kwa ajili ya kuitumikia kwenye michuano ya kimataifa na Ligi Kuu ya Vodacom Tanznaia bara.

HAYA NDIO MAJIBU ALIYOYATOA Mh MIZENGO PINDA BUNGENI MAPEMA LEO ASUBUHI


Kikao cha Bunge leo Novemba 27 kimeanza kwa maswali mawili kuulizwa na Kiongozi wa Kambi ya Upinzani Bungeni Freeman Mbowe kwa Waziri Mkuu Mizengo Pinda.

“…Chini ya uongozi wako kama Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na ukiwa kiongozi wa shughuli za Kiserikali Bungen, tumeiona Serikali ikikumbana na matatizo na vikwazo vingi ikiwemo ‘Operesheni Tokomeza’ ambayo ilipelekea wananchi wengi kupoteza maisha na wengine kupata vilema…“– Mbowe.

"Tumeona mauaji ya raia yakiendelea Kiteto, kashfa kubwa ambayo iko current sasa hivi ikiwa ni pamoja na kauli zako ulizowahi kuzisema kwamba fedha zilizopotea za akaunti ya Escrow hazikuwa fedha za umma bali zilikuwa fedha za watu binafsi…“– Mbowe.

"Baada ya Ripoti ya CAG kutolewa hadharani kuhusiana na fedha za Escrow na baada ya Ripoti ya PCCB kutolewa na hatimaye jana hapa Bungeni kusomwa taarifa ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali, nini msimamo wako kuhusu kauli yako ya awali kwamba fedha zile zilikuwa ni za watu binafsi na sio fedha za umma?“– Mbowe.

"Kwa uzito huo ukichanganya na matukio mengine mbalimbali ambayo yamepelekea fedheha kubwa kwa taifa letu, huoni kama ingekuwa muafaka kwako binafsi na taifa kupumzika kidogo ili kupisha nafasi kwa watu wengine kuweza kumalizia ngwe hii ya utawala wenu?”– Mbowe.

Akijibu maswali hayo, Waziri Mkuu Mizengo Pinda amesema; “…Inawezekana Mheshimiwa Mbowe una shauku ya kutaka litokee hilo lakini mambo haya yanategemea kama ndivyo Mungu kapanga au hapana…“

"Ningeweza nikajaribu kukujibu lakini sina sababu ya kufanya hivyo, sina sababu ya kufanya hivyo kwa sababu suala lenyewe ndiyo subject ya mjadala hapa Bungeni ambao unaanza leo.. Tusubiri mjadala utakavyokwenda naamini na mimi nitapata nafasi ya kusema mawili matatu, kwa hiyo nadhani mwisho wa yote Bunge litakuwa limefikia mahali ambapo tunaweza tukasema kwa uhakika ni hatua stahiki namna gani inaweza kuchukuliwa…” Waziri Mkuu Mizengo Pinda.

ESCROW NDO MPANGO WA MJINI



RUTI MPYAAAAAAAAA...
KITU CHA T/ESCROW KKOO NAULI 400 KAMA KAWA

MTATIRO: NCHI IMEOZA HADI ALTARENI

                              Askofu Kilaini

HII NI KAULI ALIYOITOA JULIUS MTATIRO BAADA YA VIONGOZI WA DINI KUWA KWENYE LIST YA WALIOPATA MGAWO WA MABILIONI YA ESCROW
Tunapokuwa na nchi iliyooza, viongozi wa dini wako mstari wa mbele kuchukua milungula na hela za rushwa zilizojaa damu na mateso ya kodi za wananchi.Ni aibu mno, sielewi hawa maaskofu wangu wanasimama kwenye altare kufanya nini...ni kufuru na aibu kwa mimi Mkatoliki na wakatoliki wote duniani.
Wakati Bunge linafukuza wezi, ni muhimu na Kanisa Katoliki lifukuze hawa maaskofu walafi na kuwapeleka mahakamani. Kisha kanisa lijivue ushenzi huu, lirejeshe pesa hizi kwa niaba ya watumishi hawa walafi wa fedha na mafisadi.
Shame on you beloved bishops, my bishops... 
#BishopMethodius #Kilaini & #BishopEusebius #Nzingilwa. 
#IPTL & #ESCROW #BringBackOurMoney.

SHILOLE TOTO LA KINYAMWEZI LATUA UBELGIJI....CHEKI MAFOTO YAKE HAPA ALIVYOPOKELEWA...










BREKI ZA NDEGE ZAGANDA BAADA YA KUPIGWA NA BARIDI KALI


Abiria waliokuwa wanafanya safari na shirika la ndege la Serbia walilazimika kushuka katika ndege hiyo na kuisukuma baada ya breki zake kuganda na kushindwa kuondoka.
Ndege hiyo ilikuwa inaanza kuruka kutoka katika mji wa Kirusi wa Igarka,lakini ilishindwa kusogea baada ya hali ya hewa kuwa -52C.
Abiria waliokuwa ndani ya ndege hiyo idadi yao kubwa walikuwa wafanyakazi wa ndege hiyo waliombwa kutoa msaada wa dharura wa kuisukuma ndege hiyo kwa hofu ya kutowachelewesha endapo watasubiri msaada Zaidi.
Ndege hiyo ya shirika la ndege la Katekavia baada ya muda ilimudu kuendelea na safari zake na baadaye kutua salama katika mji wa Krasnoyarsk.kwa muujibu wa mashuhuda wa tukio hili kiwango cha baridikwa muujibu wa mashuhuda wa tukio hili ,wanaeleza kuwa kiwango cha baridi kilishuka hadi kufikia nyuzi joto 52, na kugandisha mfumo wa breki za ndege hiyo .
Mkuu wa kitengo cha huduma za ndege hiyo Oxana Gorbunova, anaeleza kwama abiria hawakulazimishwa kuisukuma ndege hiyo bali kwa hiyari waliamua kusaidia kuisukuma ,japokuwa kitendo hicho hakiruhusiwi kwakuwa kitendo hicho kinaweza kuathiri bodi ya nje ya ndege hiyo ,na wanasheria nao wanachunguza endapo uwanja wa ndege,shirika la ndege,wafanyakazi wa ndege ama abiria endapo wamevunja sheria za usalama wa anga.
Uwanja huo wa ndege unatumiwa na abiria takribani elfu moja kwa mwaka ,wengi wao hufanya kazi katika makampuni ya mafuta yanayomilikiwa na Urusi.
CHANZO:BBC

MAMA MJAMZITO AMPIGA TAFU MUMEWE KUBAKA BINTI WA MIAKA 7


Mwanamke mmoja nchini China ambaye ni mjamzito amehukumiwa kifungo cha maisha huku mume wake akihukumiwa adhabu ya kifo baada ya kushirikiana kumbaka na kisha kumuua msichana wa miaka17.
Mwanamke huyo ambaye anajulikana kwa jina la Tan Beibei alifanya kitendo hicho baada ya msichana huyo kumsaidia alipoanguka barabarani ambapo alimpeleka hadi nyumbani kwake na badala ya kumshukuru waliamua kumfanyia kitendo hicho cha akishirikiana na mumewe kisha kumuua na kuamua kumzika.
Mahakama ya Heillojiang ya nchini humo imesema kuwa imewafungulia mashtaka ya kuua,kubaka pamoja na kushambulia baada ya mwanamke huyo kujifanya ni mgonjwa na kushirikiana na mumewe kumfanyia binti huyo kitendo hicho cha kudhalilisha kisa wivu kwa madai alikua akitembea na mumewe.
Mahakama ya juu ilikataa kuwapunguzia adhabu wawili hao baada ya kukata rufaa kwa madai kesi hiyo ni kubwa na haina dhamana yoyote.
Kwa mujibu wa mashuhuda msichana huyo aliyejulikana kwa jina la Hu alikua akipita barabarani ndipo mama huyo alipomwomba msaada wa kumpeleka nyumbani kwake baada ya kuanguka na msichana huyo kutii lakini alipofika alikutana na maswaiba hayo.
Inaelezwa kuwa baada ya kufika mume wa mwanamke huyo alimpa msichana huyo maziwa ya mtindi na baadaye kuanza kumfanya kitendo hicho lakini hata hivyo hawakufanikiwa kwani binti huyo aliweza kuwazidi nguvu na walipoona imeshindikana walichukua blanketi na kumziba nalo usoni hadi alipofariki dunia na kuamua kumzika.
Katika utetezi wa mwanamke huyo mahakamani hapo alisema aliamua kufanya kitendo hicho kwa sababu binti huyo alikua akitembea na mume wake.
Historia inaonyesha wawili hao walishawahi kuwa na kesi mbalimbali kiwemo ya kutaka kumbaka rafiki wa mtoto wao wa kike ambaye alikua akisoma naye darasa moja.

BAADA YA KIM KARDASHIAN SASA NI ZAMU YA WIZ KHALIFA KAJIFOTOA MTUPUUUUUUU AKIWA BAFUNI


Ikiwa zimepita siku kadhaa tangu Supastaa Kim Kadarshian kukaa kwenye vichwa vya habari vya mitandao mbalimbali kutokana na picha zake zikimuonyesha akiwa tupu kuzagaa kwenye mitandao, staa mwingine tena huenda akaingia kwenye list ya #BreaktheInternet.
Kwenye ukurasa wa Rapa Wiz Khalifa ameweka picha inayomwonyesha akijimwagia maji kichwani huku akiwa mtupu ndani ya bafu.
Bado haijafahamika kama amefanya hivyo kama njia ya kuyatangaza maji hayo au ana maana ipi.

KASHFA YA MISS TANZANIA 2014,UTATA MPYAAAAAAA WAIBUKA


Hatima ya kashfa ya kudanganya umri inayomkabili aliyekuwa mrembo wa Tanzania mwaka 2014, Sitti Mtemvu bado ipo kizani baada ya polisi kuikana kauli ya Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (Rita).

Rita, kwa upande wao ilieleza wiki moja iliyopita kuwa imekabidhi polisi vielelezo kuhusu uchunguzi wa kashfa hiyo kwa lengo la kuchukua hatua.

Juzi, Kamishna wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova alikana kupokea taarifa za vielelezo hivyo vilivyotumiwa kuombea cheti cha kuzaliwa cha Sitti Mtemvu.

Wiki mbili zilizopita, Wizara ya Habari, Utamaduni, Vijana na Michezo kupitia Baraza la Sanaa la Taifa (Basata) ilijivua lawama katika kashfa hiyo na kuiachia Rita.

Akizungumza na gazeti hili juzi, Kova alisema, “Jeshi la Polisi halijapokea vielelezo vyovyote kutoka Rita, wamepeleka wapi? Iwapo waliviwasilisha katika kituo chochote cha polisi watoe taarifa iliyo sahihi, iwapo vielelezo hivyo vitatufikia tutachukua hatua stahiki,” alisema Kova.

Kwa upande wao, Rita waliahidi kuwasilisha vielelezo hivyo wiki hii na kwamba vilicheleweshwa kutokana na kukamilisha upekuzi wa taarifa za kuombea cheti pamoja na cheti cha awali kilichokuwa kikitumiwa na Sitti Mtemvu.

Mkurugenzi wa Idara ya Sheria wa Rita, Emmy Harrison alisema jana kuwa idara yake imekamilisha taratibu zote zinazotakiwa na vielelezo hivyo vitakabidhiwa rasmi polisi.

“Haya ni masuala ya kisheria, hivyo sisi tumeshakamilisha kile tulichotakiwa kukifanya na mchakato huu bado unaendelea, tupo katika maandalizi ya mwisho kwa ajili ya kuripoti polisi, wiki hii vielelezo vya Sitti vitapelekwa kwenye vyombo vya usalama kwa ajili ya hatua zaidi,” alisema Harrison.
CHANZO: MWANANCHI

MRITHI WA JAJA HUYOOOOOOOOO KASHATUA.......



Nyota mpya wa Klabu ya soka ya Yanga ya Dar es Salaam, anayekuja kufanya majaribio ya kuziba nafasi ya Mbrazil mwenzake Genlson Santos 'Jaja', Emerson De Oliveria Neves Rouqe akitoa ishara ya dole mara baada ya kuwasili uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere (JNIA) Dar es Salaam na kupokelewa na viongozi wa Yanga. 
Rouque aliwasili na Kocha mkuu wa Yanga, Marcio Maximo pamoja na Nyota mwingine kutoka Brazili Andrew Coutinho.

ICHEKI SURA YA YULE BEKI TATU WA UGANDA BAADA YA KUPOKEA KICHAPO HEVI



Huu ndio muonekano wa yule msichana wa kazi za ndani aliye tenda unyama wa kutaka kumuua mtoto wa bosi wake atimaye naye amepokea kipigo takatifu cha nusu kufa kutoka kwa wazazi wa uyo mtoto hii ni moja ya picha zilizo vuja ambazo wazazi wa mtoto family iyo walizificha.

VYUO VIKUU TANZANIA HOVYO KABISA....VYAIAIBISHA NCHI...


Vyuo vikuu vitatu vya Tanzania ambavyo vilishiriki katika mashindano ya mjadala wa Afrika kuhusu Sheria za kimataifa za haki za kibinaadamu yalioandaliwa na kamati ya kimataifa ya shirika la msalaba mwekundu ICRC vimeshindwa kufika katika raundi ya mwisho.

Badala yake vyuo hivyo viliondolewa katika raundi za mapema ambapo mataifa manane ya Afrika yalishiriki.

ICRC imekuwa ikiandaa hafla kama hizo kwa kipindi cha miaka 14 sasa mjini Arusha.

Kulingana na gazeti la the Citizen nchini Tanzania, vyuo vilivyoiwakilisha Tanzania ni chuo cha kanisa katoliki cha Ruaha kutoka Iringa,Chuo cha Iringa na Chuo kikuu cha Zanzibar.

Katika raundi ya mwisho ya mashindano hayo yaliofanyika mwishoni mwa wiki katika mahakama maalum ya kimataifa inayochunguza mauaji ya kimbari nchini Rwanda ICTR mjini Arusha,chuo cha Strathmore University kutoka Kenya kiliibuka mshindi na kufuatiwa na chuo cha Christian University kutoka Uganda huku chuo cha Kunduyi pasi kutoka Zimbabwe kikiibuka mshindi wa spika bora.

Raundi ya mwisho ya mjadala huo ilisimamiwa na jaji wa mahakama hiyo Vagn Joensen,jaji wa mahakama kuu ya Tanzania Stella Mugasha,jaji wa mahakama ya haki katika Afrika mashariki Fanstin Ntezilyayo,John Joseph Wamwara na Mutsa mangezi kutoka ICRC.

Judge Joensen, ambaye alitoa zawadi kwa washindi aliyapongeza mashindano hayo kama kifaa cha kuwahamasisha wanafunzi wa vyuo vikuu wanaofanya sheria na kwamba itasaidia kuimarisha maono yao katika siku za usoni.

UBAGUZI WA RANGI WAKITA MIZIZI MAREKANI....WATU WEUSI WAWEKWA GEREZANI,WAHUKUMIWA KIFO NA WENGINE WAPIGWA RISASI NA POLISI


Mkuu wa Haki za Binaadamu Katika Umoja wa Mataifa ameelezea wasiwasi wake kuhusu 'ubaguzi uliokita mizizi' na idadi kubwa kupita kiasi ya Wamarekani weusi au wenye asili ya Afrika ambao wanauawa na polisi nchini Marekani.

Zeid Ra’ad Al Hussein Kamishna wa Haki za Binadamu katika Umoja wa Mataifa ameongeza kuwa kuna idadi kubwa kupita kiasi ya Wamarekani weusi wanaoshikiliwa gerezani na wanaosubiri kutekelezwa hukumu za kifo dhidi yao.

Matamshi hayo yametolewa kufuatia ghasia kubwa zilizoibuka baada ya jopo la mahakama huko Missouri, Marekani kumuondoa hatiani afisa mzungu wa kikosi cha polisi ambaye alimpiga risasi na kumuua kijana Mmarekani mwenye asili ya Afrika, Michael Brown, katika mji wa Ferguson. Ghasia zimeripotiwa katika miji zaidi ya 90 kote Marekani ambapo waandamanaji wanalalamikia ukandamizaji na ubaguzi wa wazi dhidi ya watu wenye asili ya Afrika katika mfumo wa utawala nchini Marekani. Gavana wa Jimbo la Missouri, Jay Nixon, ameagiza wanajeshi wengine 2,200 wa Gadi ya Taifa kupelekwa Ferguson kukabiliana na waandamanaji wenye hasira.

MTI ULIOINUKA BAADA YA KUANGUKA MIAKA 3 ILIYOPITA WAENDELEA KUFANYA MAAJABU


Mti huo umeinuka siku ya Oktoba 15 mwaka huu, ambapo Katibu tawala wa Wilaya ya Uyuwi amesema;
 “…kwa mazingira tunayoyaona hapa tukio ni kweli limetokea sasa ni kwa nguvu zipi kwa uwezo wa Mungu au nguvu za giza hili nadhani kwa sasa litakuwa hatuwezi kulitolea taarifa ,lakini cha msingi eneo hili tulitunze kwa matumizi ya kumbumbuku ya vizazi vyetu na pamoja na wengine watakaotoka nje ya eneo hili, ambao watataka kuja kuona maajabu ya Mwenyezi Mungu tofauti na kule Mfuto ulipoinuka tu siku ya pili yake tukakuta kila kitu hakuna, kwa hiyo nilikuwa napenda niwapongeze Wanakijiji kwa kulinda Mti huu…”

Shuhuda wa kwanza kuzungumzia tukio hilo amesema; “… Haya magome ya mzizi yakichimbwa, yakisagwa mtoto akiwa anaumwa Degedege wakimvutisha ile hali ya mchango inashuka hata kama unaumwa kipanda uso, hata kama unaumwa kichwa cha kawaida…”

Mwanakijiji mwingine amesema; “…Huu Mti kama mbwa wako sio mkali unachimba mizizi unakoboa magome unatwanga ule unga wake unamnusisha kwenye pua anakuwa mkali sana…“

Mtu mwingine amesema; “Kama kuna Mtu ambaye pengine kashaishiwa pengine fahamu wanajaribu kumuwekea puani na mara anapiga chafya…”

Mh MKONO HAKULISHWA SUMU


         Mh.Nimrod Mkono (MB).

Siku chache baada ya Mbunge wa Musoma vijijini Nimrodi Mkono kusema amelishwa sumu akiwa London Uingereza,Mbunge wa Chadema Halima Mdee amemtaka kusema ukweli na si kulihadaa Taifa kwa uongo.
Mkono alisema leng la kulishwa sumu ni kutaka kuharibu figo zake ndani ya saa72 lakini kitendo hicho kilichoshindikana.
Mdee aliyekua na Mkono katika ziara hiyo nchini Uingereza alisema hakuna ukweli wowote kuhusu yeye kutaka kulishwa sumu,nilikua naye kule na mazingira ya kuanza kuumwa hadi kupona kwake ni utata mtupu….awaeleze Watanzania anaumwa nini na si kusingizia alilishwa sumu,”alisema.
‘Kama anataka kutumia kivuli cha Escrow,arudi bungeni tuweze kujadili na tuimalize ili asiseme kuwa sijui wanataka kumuua ni uongo.

RICK ROSS APATA DEMU MPYAAAAAAAA BONGE LA TAJIRI....



Rick Ross The Boss ambaye aliwahi kuja Tanzania kwenye Fiesta, juzi kati alifanya party ya kusherehekea album yake mpya ya Hood Billionaire huko Atlanta Georgia Marekani.
Unaambiwa kwenye party hiyo Rozay alikua bega kwa bega na mrembo Ming Lee ambaye anatajwa kuwa milionea kutokana na biashara ya nywele na kampuni yake ambayo inahusisha pia nguo na Salon.
Baada ya kuonekana pamoja zimeanza kusambaa fununu kwamba Rozay ndio kajiegesha hapo kwa sasa.