Saturday 22 November 2014

BONDIA MTANZANIA NA MANNY PACQUAIO KUPANDA ULINGONI USIKU WA LEO


BONDIA wa Tanzania wa Ngumi za Kulipwa, Fadhil Majia usiku wa leo Jumamosi anatarajia kupanda ulingoni nchini China kuzichapa na Jerwin Ancajas katika pambano la utangulizi la kimataifa kati ya Mfilipino, Manny Pacquaio na Cris Ageiri.

Tanzania ndiyo nchi pekee kutoka Afrika yenye bondia katika pambano hilo kubwa duniani litakalofanyika kwenye Ukumbi wa Cotai Arena, Venetian Resort, Macao humo.Akizungumza na Championi Jumamosi, Katibu wa Shirikisho la Ngumi za Kulipwa Tanzania (PST), Anthoy Rutta, alisema Manny Pacquiao na Fadhili Majia wamepima uzito jana usiku tayari kwa pambano hilo.

“Mabondia wote watakaocheza kwenye pambano la Jumamosi (leo) wamepima uzito na afya zao usiku wa jana akiwemo Manny Pacquaio na Mtanzania Fadhil Majia tayari kwa kazi hiyo.

“Majia ndiye atakuwa bondia wa kwanza kucheza pambano la utangulizi na Jerwin Ancajas, pia ni bondia pekee anayetokea barani Afrika, hivyo tunamtakia kila la kheri katika pambano lake,” alisema Rutta.  
Source: Gazeti la Champion Jumamosi

CHANONGO AGOMA KUICHEZEA SIMBA,KISIGA AULILIA UONGOZI


Kiungo wa Simba, Shaban Kisiga ameupigia magoti uongozi wa timu hiyo akiomba umrudishe kwenye timu huku kiungo mshambuliaji, Haruna Chanongo akigoma kuichezea timu hiyo.

Hivi karibuni uongozi wa Simba uliwasimamisha wachezaji watatu, Amri Kiemba, Kisiga na Chanongo kufuatia madai ya utovu wa nidhamu na kucheza chini ya kiwango kwenye mechi dhidi ya Tanzania Prisons katika matokeo ya bao 1-1.

Aidha, kwa upande wa Kiemba, uongozi wa Simba upo katika mazungumzo ya kumuuza mchezaji huyo kwa Azam FC ambapo wanataka walipwe kiasi cha shilingi milioni 15 badala ya milioni 10 wanayoitaka wao.

Kikizungumza na Championi Jumamosi, chanzo cha kuaminika kutoka Simba kimefunguka kuwa, Kisiga ameamua kuuomba msamaha uongozi wa klabu hiyo kufuatia kosa la utovu wa nidhamu alioufanya ambapo tayari amesharudishwa kundini kujiunga na wenzake.

Kilieleza kuwa, kwa upande wa Chanongo, amegoma na hataki kuisikia Simba wala kuichezea tena na badala yake anahitaji aachwe, hivyo kuwapa wakati mgumu viongozi wa timu hiyo.

“Kuhusu Kisiga ishu yake iliisha zamani, aliomba msamaha kwa utovu wa nidhamu alioufanya kwa hiyo ataungana na wenzake mara baada ya kikosi kuanza mazoezi.

“Kwa upande wa Chanongo suala lake linaonekana kuwa gumu, mwenyewe hataki kuichezea Simba, haijajulikana nini hatma yake kwani kuna baadhi ya viongozi wanapendekeza arudishwe Simba B lakini bado hatujaafiki suala lake,” kilisema chanzo hicho.
SOURCE: GPL

MAGAZETI YA UDAKU NA MICHEZO LEO HII JUMAMOSI NOVEMBA 22


















MAGAZETI YA BONGO LEO HII JUMAMOSI NOVEMBA 22



















JOKATE NA GAETANO KUFANYA KIPINDI KIPYA NDANI YA M Net EAST AFRICA


Mbunifu wa mitindo na muigizaji wa filamu nchini, mrembo Jokate Mwegelo kwa kushirikiana na mshiriki maarufu wa Big Brother Africa, Mganda Gaetano Kagwa wameteuliwa kuendesha kipindi kipya cha Maisha kijulikanacho kwa jina la “Beat the Challenge” kupitia M-Net East Africa.
Kipindi kitashindanisha familia mbalimbali katika nchi za Tanzania, Kenya na Uganda na mshindi atapewa gari jipya kabisa kutoka kwa waandaaji.  Katika mashindano hayo, kila  familia inatakiwa kuwa na watu wanne ambao ni Baba, Mama na watoto wawili wenye umri kati ya miaka 12 na 17.
Familia hizo zitashinda katika kutatua changamoto mbalimbali zitakazowasilishwa na waandaaji na kila familia itakuwa na jukumu la kutatua hizo changamoto kwa kutumia nguvu kuliko ufahamu wa akili.
Akizungumza jana Jokate alisema kuwa amejisikia faraja kubwa kupewa nafasi hiyo ambayo itampa uzoefu zaidi katika fani ya utangazaji na kujipanua kimawazo.
Jokate ambaye pia ni Miss Tanzania namba mbili wa mwaka 2006 alisema kuwa anajisikia faraja kubwa kwa kuzidi kuongeza wigo wa mawasiliano kwani hii si mara yake ya kwanza kuendesha vipindi katika televisheni baada ya kutamba katika kipindi cha Chaneli O.
“Kama nilivyosema, nataka kuishi kwa kutegemea vipaji vyangu na wala si vinginevyo, nimeanza katika urembo, nikaja katika ubinifu na uanaminitindo, MC, muigizaji wa filamu na sasa mtangazaji, kote huko nimefanikiwa, ni faraja kubwa kwangu,” alisema Jokate.
Alisema kuwa anashukuru kuona kuwa filamu yake ya Mikono Salama kwa sasa inatamba sana na inamuongezea sifa kubwa katika fani hiyo. “Hata kidoti Fashion nayo inatamba, hivyo kwa nashukuru Mungu kwa kuniwezesha,” alisema.
Kwa upande wa Tanzania, utafutaji wa washiriki utafanyika Jumamosi Novemba 22), New Africa Hotel, wakati Uganda watafanyia kwenye hotel ya Silver Springs, Kampala na Kenya kwenye studio za Supersport zilizopo katika Barabara ya Jamhuri.
Kipindi cha kwanza kitarushwa Desemba 13 kupitia chaneli ya Maisha Magic 161 kuanzia saa 2.30 usiku kwa mujibu wa Jokate.

MISS SINZA APIGA TENA PICHA ZA UCHI


Miss Sinza 2001 na aliyekuwa mshiriki wa Miss Tanzania 2011, Husna Maulid ameonesha kuwa ni sikio la kufa baada ya kupiga picha za utupu kwa mara nyingine.



Picha hizo zilizotapakaa kwenye mitandao mbalimbali zimewashangaza watu ambapo Husna anaonekana akiwa kama alivyozaliwa huku akiwa katika mapozi tofauti hali inayoonesha kwamba alikuwa akipigwa picha hizo na mpenzi wake.

Kwa mujibu wa mdau ambaye aliziweka picha hizo kwenye mtandao wa Instagram, mwanadada huyo alipigwa picha hizo na mpenzi wake ambaye hakumtaja jina.Alisema mpenzi wake huyo alimuomba ampige picha ili awe anaziangalia kila wakati kwani anampenda sana ambapo Husna alikubali kupigwa picha hizo lakini matokeo yake zikazagaa mitandaoni.

KASHFA YA IPTL & ESCROW YAPELEKEA NIMROD MKONO KULISHWA SUMU UINGEREZA

Mh Nimrod Mkono (Mb) amekoswakoswa kuuawa nchini Uingereza alikokuwa amekwenda kikazi. Aliwekewa sumu ambayo ilipaswa iharibu kabisa figo zake ndani ya saa 72. Uongozi wa bunge umethibitisha na ripoti ya madaktari wa London inaonesha hivyo.

Mkono mwenyewe anasema alionywa kuwa usalama wake uko mashakani na akatakiwa asifikie katika hoteli ambayo ujumbe wa viongozi wa Tanzania utafikia.
Mkono anasema alipofika London aliamua kwenda katika nyumba yake binafsi, lakini baadaye alianza kutoka jasho, kuishiwa nguvu na kupoteza fahamu kwa saa 6.

Ikumbukwe kuwa Mkono na kampuni yake ya Mkono & Advocates ndiyo iliyokuwa inatetea upande wa TANESCO na Serikali katika kesi dhidi ya IPTL.
Inasemekana Mkono anatafutwa kuuawa kwa sababu inaonekana ana taarifa nyingi mno kuhusu sakata la IPTL na ESCROW, na serikali inamtuhumu kuwa yeye ndiye aliyevujisha nyaraka zote hadi umma wa watanzania kugundua kuwa zaidi ya bilioni 321 mali ya umma zimeibiwa katika sakata hilo.
CHANZO: GAZETI LA THE CITIZEN

POLISI ALIYEMUUA MWANAFUNZI CHUO KIKUU JIJINI MBEYA APEWA HUKUMU YA KIFO


MAHAKAMA Kuu Kanda ya Mbeya imemhukumu kunyongwa hadi kufa polisi wa upelelezi, Maduhu, F 5842, aliyekuwa akikabiliwa na shitaka la mauaji ya mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Teofilo Kisanji (TEKU), Daniel Mwakyusa.

Aidha, mahakama hiyo imewaachia huru washitakiwa wengine wawili wa kesi hiyo, polisi wa upelelezi, Shaaban, F 7769, na polisi wa kike mpelelezi, Neema, F 6545, baada ya kuwakuta hawana hatia.

Hukumu hiyo ya kesi namba 16 ya mwaka 2013, ilitolewa jana mjini hapa na Jaji Rose Temba, baada ya kuridhishwa na ushahidi uliotolewa na pande zote mbili.

Awali, ilielezwa mahakamani hapo na mawakili wa serikali, Archiles Mulisa akisaidiwa na Catherine Paul kuwa washitakiwa walifanya mauaji ya kukusudia Februari 14 mwaka 2012 kinyume cha Kifungu Namba 196 cha Kanuni ya Adhabu sura ya 16 kama ilivyofanyiwa Marejeo mwaka 2002.

Mulisa alidai washitakiwa hao kwa pamoja walihusika na mauaji ya Daniel Mwakyusa baada ya kumpiga kwa kutumia silaha inayodhaniwa kuwa ni bunduki, nje ya ukumbi wa starehe wa Universal uliopo Uyole jijini Mbeya.

Akitoa hukumu ya kesi hiyo, Jaji Temba alisema anawaachia huru mshitakiwa namba mbili, Shaaban ambaye alikuwa dereva wa gari ya polisi kwa kuwa ushahidi uliotolewa, unadhihirisha kuwa alibaki ndani ya gari akimsubiri mshitakiwa namba moja aliyeshuka na kuingia kwenye ukumbi wa Universal.

Kwa upande wa mshitakiwa namba tatu, Neema, Jaji Temba alisema aliridhishwa na mshitakiwa huyo kutohusika na mauaji kwa kuwa siku ya tukio alikuwa akijisikia vibaya, hivyo alilazimika kubaki na dereva kwenye gari.

Jaji Temba alisema mshitakiwa namba moja, Maduhu, anahusika moja kwa moja na mauaji hayo, kutokana na ushahidi wa kimazingira, kwani yeye ndiye aliyekuwa mtu wa mwisho kuondoka na Daniel Mwakyusa eneo la tukio na kumpeleka kwenye gari.

Alisema sababu ya pili, ushahidi ulionesha kuwa silaha yake pekee ndiyo iliyotumika, tofauti na za askari wengine kwa kuwa risasi tatu zilionekana kupungua kati ya zile alizokabidhiwa sambamba na ushahidi wa maganda matatu ya risasi, yaliyookotwa eneo la tukio.

Jaji Temba alisema sababu ya tatu ni kuwa ushahidi uliotolewa, unaonesha kuwa mshitakiwa huyo alikuwa wa mwisho kurejesha silaha, hivyo kuhusishwa moja kwa moja na mauaji hayo.

Alisema kutokana na sababu hizo, mahakama inamtia hatiani kwa kuua kwa kukusudia, hivyo mshitakiwa Maduhu, amehukumiwa kunyongwa hadi kufa.

Awali, ilidaiwa kuwa siku ya tukio ilikuwa Siku ya Wapendanao (Valentine’s Day), ambapo mtuhumiwa akiwa doria na askari wenzie, alimkuta Daniel Mwakyusa akiwa kwenye eneo la starehe na mwanamke anayesadikiwa kuwa alikuwa pia na mahusiano na askari huyo.

MFUMO MPYA WHATSAPP WAVUNJA NDOA ILIYODUMU MIAKA 2


Wiki chache baada ya WhatsApp kutambulisha mfumo mpya ambapo iwapo unamtumia message mtu inakuonyesha alama ya tick mbili za kijani na pia inaonyesha muda ambao mtu uliyemtumia message hiyo ameisoma, tayari kuna ndoa ambayo imeingia matatizoni kutokana na hilo.
Mwanaume mmoja Saudi Arabia ametoa talaka kwa mkewe kutokana na kitendo cha mwanamke huyo kutokujibu message aliyomtumia WhatsApp.
Mwanaume huyo amesema kitendo kilichomkasirisha zaidi ni pale aliporudi nyumbani na kumkuta mke wake akiwa busy anachat na marafiki zake kupitia mtandao huo wakati message aliyomtumia yeye hakuijibu.

Jamaa huyo ameona kama kitendo hicho ni dharau kubwa na hakuwa tayari kuendelea na ndoa hiyo ambayo imedumu kwa miaka miwili tangu ifungwe.

ARSENAL YAWAKOSA MESSI NA PIQUE


Kocha wa klabu ya Arsenal Arsene Wenger amethibitisha kuwa kilabu hiyo ilijaribu kumsajili nyota wa kilabu ya barcelona Lionel Messi kama mpango wa kutaka kuwanyakua wachezaji watatu wachanga wa kilabu hiyo.

Messi alikuwa na miaka 15 wakati huo na mwenzake Gerrad Pique pamoja na aliyekuwa kiungo wa kati wa Arsenal Cess fabregas.

Wenger:''Tulitaka kumchukua Fabregas,Messi na Pique,lakini tukafanikiwa kumpata Fabregas pekee''.

Fabregas aliichezea kilabu ya Arsenal kwa miaka minane kabla ya kurudi Barcelona ,huku Pique akijiunga na Manchester United mwaka 2004.


Messi mwenye umri wa miaka 27,ameichezea timu ya Barcelona kwa muda wote na kuisadia kushinda mataji sita ya La liga pamoja na kombe la vilabu bingwa mara tatu baada ya mpango wa kujiunga na Arsenal kugonga mwamba.

Hatahivyo ,Wenger amepinga madai kwamba mpango huo ulifeli kutokana na makaazi ya Messi na familia yake. Mchezaji huyo wa timu ya Argentina pia angelazimika kuwa na kibali cha kufanya kazi nchini Uingereza.

Wenger aliongezea:''Nadhani Messi mwenyewe hakutaka kujiunga nasi''.

BAADA YA KUKATALIWA KUPANDA NDEGE KWENDA INDIA KWA MATIBABU,KIJANA WA KITANZANIA AFARIKI DUNIA


Sande Jacob Mremi (pichani) amefariki Siku chache baada ya kukosa usafiri wa ndege ambapo alitakiwa kwenda nje ya nchi kupata matibabu.
Kituo cha ITV kiliripoti kuhusu habari za kijana huyo kuumwa na kutokana na kusumbuliwa tatizo la uzito mkubwa nakushindwa kupata Ndege ya kumsafirisha kwenda kwenye matibabu India kijana huyo amefariki Dunia.
Ndugu wa kijana huyo walilalamika kutoridhishwa na baadhi ya Mashirika ya Ndege kwa kushindwa kuwasaidia kumsafirisha ndugu yao.
Katika mahojiano na ITV mama wa mtu huyo amesema; “..yaani kwa kweli mashirika ya Ndege hayakuweza kutufanyia haki kwa kweli, wametunyanyasa kwa sababu tulipokuwa tunapeleka maombi tunataka kumsafirisha mtoto wetu ilikuwa wao watusaidie na kutupa maelekezo tunatakiwa tufanye nini na nini, lakini baada ya kuona tunakosa msaada ndio tukaamua kuja ITV ili watusaidie, kwa hiyo yeye mwenyewe akaanza kupata presha kwa sababu presha alikuwa hana mpaka anapanga kusafiri alikuwa hana presha nilimpima vipimo vyote alikuwa hana tatizo lolote…”
Dada wa marehemu amesema; “..Ethiopia walitusaidia kwa kweli mpaka hatua ya mwisho na Jumapili kama Mungu angemuweka hai Ethiopia wangemsafirisha, na mashirika ya Ndege mengine yalitakiwa yatuelekeze hivi, lakini sasa kutokana na ile hali mara leo kapelekwa kesho anarudishwa mdogo wangu kesho kutwa kapelekwa amerudishwa mdogo wangu, msongo wa mawazo umemkaa rohoni anashindwa kuongea maskini ya Mungu, mawazo paka yamemfanya mdogo wangu alikuwa hana presha paka presha imekuja paka mdogo wangu anafariki.

Baba wa Sande amesema; “…wakatumia sheria ya pili ya kunihusisha mimi wakaniambia bwana kumbe mtu huyu ni mkubwa sana tunatakiwa tuvunje viti tumbebe, nikawauliza nikulipeni bei gani? wakaniambia tulipe dola elfu saba mia tano na thelathini na nne, na mara ya kwanza tulilipa dola elfu sita miambili ishirini…”
Bado haijafahamika kama Shirika hilo la ndege litarudisha hela ambayo ililipwa na watu hao kwa ajili ya kumsafirisha ndugu yao.

KAIMU RAIS WA ZAMBIA ATIMULIWA CHAMANI


Chama tawala nchini Zambia (PF) kimemtimua kaimu rais wa nchi hiyo Guys Scott kutoka chamani na kuvunja utaratibu wa katiba.

Taarifa hii ni kwa mujibu wa msemaji wa chama hicho.

''Amekuwa akiwaajiri na kuwafuta watu kazi ovyo na pia bila ya kushauriana na kamati kuu ya chama,'' amesema Malozo Sichone.

Bwana Scott, ambaye licha ya hatua hiyo ataendelea kuwa mwanachama wa chama hicho, ataendelea kuhudumu kama kaimu rais hadi uchaguzi utakapofanyika tarehe 20 Januari.

Scott aliteuliwa kuwa kaimu rais kufuatia kifo cha hayati Rais Michael Sata aliyefariki mwezi jana.

RATIBA YA LIGI KUU UINGEREZA LEO HII


Chelsea v West Brom18:00

Everton v West Ham18:00

Leicester v Sunderland18:00

Man City v Swansea18:00

Newcastle v QPR18:00

Stoke v Burnley 18:00

Arsenaly v Man Utd 20:30

Mechi zote kuchezwa saa za Afrika Mashariki

Friday 21 November 2014

RONALDO AOSHA VYOMBO BAADA YA KUSHINDWA KAMARI


Aliyekuwa mchezaji wa timu ya Brazil Ronaldo alilazimika kuosha vyombo baada ya kushindwa katika mchezo wa karata na mchezaji wa tennisi Rafa Nadal,na kumfanya mchezaji huyo wa tenisi kupokea dola 50,000 za hazina yake ya kutoa msaada huku Ronaldo akiosha vyombo.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 38 alikabiliana vilivyo na mwana tenisi huyo kutoka uhispania katika mechi kati ya wawili hao katika meza ya pokerstar, Casino ya Hippodrome mjini London ambapo Nadal alishinda fedha hizo.

Duru ziliarifu kwamba kiini cha nyota hao wawili kukutana katika chumba kimoja ni chakula kilichoandaliwa katika hafla hiyo.

Hatahivyo kitu kilichowafurahisha wengi kulingana na wageni ni hatua ya Ronaldo kukubali kushindwa na kupewa kazi ya kuviosha vyombo vya Nadal alivyotumia kula.

MAADHIMISHO SIKU YA UKIMWI DUNIANI 2014 KITAIFA KUFANYIKA NJOMBE


Maadhimisho ya siku ya UKIMWI Duniani kwa mwaka 2014 kitaifa yanatarajiwa kufanyika mkoani Njombe kuanzia tarehe 24 mwezi huu hadi tarehe  moja  Desemba.

Hayo yamesemwa leo na Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya Taifa ya kudhibiti UKIMWI (TACAIDS) Dkt. Fatma Mrisho wakati akiongea na waandishi wa habari katika ukumbi wa mikutano uliopo makao makuu ya tume hiyo jijini Dar es Salaam.

Dkt. Mrisho alisema kauli mbiu ya maadhimisho hayo ni “Tanzania bila maambukizo mapya ya Virusi Vya Ukimwi (VVU), Vifo vitokanavyo na UKIMWI, Ubaguzi na unyanyapaa inawezekana.

“Kauli mbiu hii inalenga kutoa msukumo wa utekelezaji wa mikakati mbalimbali ya kudhibiti UKIMWI kitaifa na kimataifa ili kufikia azma ya sifuri tatu zinazomaanisha maambukizi mapya sifuri, vifo vitokanavyo na UKIMWI sifuri na unyanyapaa sifuri ifikapo mwaka 2018”.


Kauli mbiu hii pia inahimiza utekelezaji wa dhati wa malengo ya Maendeleo ya Milenia na maazimio yaliyowekwa kwenye mkutano maalumu wa Umoja wa Mataifa kuhusu UKIMWI uliofanyika mwaka 2001 nchini Marekani”, alisema Dkt. Mrisho.

Alisema kipaumbele cha maadhimisho ya mwaka huu ni upimaji wa hiari wa VVU na ushauri nasaha, na kutoa  wito kwa wananchi kujitokeza kwa wingi ili wapate huduma hii muhimu.

Aidha Mkurugenzi huyo aliwataka wananchi kuadhimisha siku hiyo kwa njia ya makongamano, kumbukumbu za waliofariki kwa UKIMWI, midahalo, mikutano ya wazi, vipindi kupitia vyombo vya habari, kutembelea na kutoa misaada kwa watoto yatima na wanaougua ugonjwa huo  na kutoa elimu inayohusu kujikinga na maambukizi.


Akizungumzia kuhusu upatikanaji wa dawa za kupunguza makali ya ugonjwa wa UKIMWI Mkurugenzi wa Sera, Mipango na Utafiti wa TACAIDS Dkt. Raphael Kalinga alisema dawa hizo hutolewa  bila malipo kwa wahitaji wanaostahili kuzipata hii ni kulingana na mfumo wa utoaji kwa wahitaji.

“Kuna baadhi ya wagonjwa hulazimisha kupewa dawa za kupunguza makali ya virusi vya UKIMWI ingawa kinga zao bado zinamudu kukabiliana na tatizo hilo wakati si sahihi kufanya hivyo. Kwani wanaostahili kupata dawa hizo ni wale ambao kinga zao zipo  chini”, alisema  Dkt. Kalinga.

Maadhimisho ya wiki hiyo yataenda sambamba na maonyesho ya shughuli za wadau wa udhibiti UKIMWI nchini na kongamano la kitaifa la kutathimini hali  na mwelekeo wa udhibiti  wa ugonjwa huo.  


11 WAPOTEZA MAISHA KANISANI

Polisi ya Zimbabwe imetangaza kuwa kwa watu 11 wamepoteza maisha kutokana na msongamano mkubwa wa watu, wakati walipokuwa wakitoka katika uwanja mmoja baada ya kumaliza ibada ya Kikristo. Shadreck Mubaiwa, Msemaji wa Polisi ya nchi hiyo amesema kuwa, watu wanne walifariki katika eneo la tukio huku wengine saba wakipoteza maisha hospitali. Ameongeza kuwa, mauaji hayo yalitokea jana usiku katika mji wenye kuchimbwa madini wa Kwekwe, yapata kilometa 220 kutoka Harare, mji mkuu wa Zimbabwe wakati idadi kubwa ya watu walipokuwa wakitoka katika uwanja wa mji huo kwa ajili ya ibada. Watu wengine wamejeruhiwa na wengine hali zao zikiwa mahututi. Inaelezwa kuwa, maelfu ya watu walikuwa wamehudhuria katika ibada hiyo iliyomalizika majira ya usiku.

23 WASHIKILIWA KWA TUHUMA ZA MAUAJI SINGIDA


JESHI la polisi mkoa wa Singida, linawashikilia watu 23 wakazi  wa kijiji cha Nkyala kata ya shelui wilaya Iramba mkoa wa Singida, kwa tuhuma ya kudaiwa kuuawa kwa makusudi wezi wanne wa madume ya Ng’ombe.

Akizungumza na waandishi wa habari jana ofisini kwake, Kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Singida, ACP, Thobias Sedoyeka, alisema watu hao kati yao 21 wanatuhumiwa kwa mauaji na wawili wanatuhumiwa kuiba ng’ombe watatu.

Aliwataja watu hao waliouawa kwa tuhuma ya wizi wa madume matatu ya ng’ombe ni Magupa Ngelela (32), Hemedi Masasi (29), wote wawili ni wakazi wa kijiji cha Nkyala.Wengine ni Saidi Hamisi (32) mkazi wa kijiji cha Kinkungu na Didas Mwigulu (36) mkazi wa kijiji cha Mgongo.

Akifafanua,alisema novemba 19 mwaka huu saa saba usiku,watu hao wanne kwa pamoja inadaiwa walivunja zizi la Omari Iddi mkazi wa kijiji cha Nselembwe na kuiba madume matatu ya ng’ombe.

Alisema asubuhi yake,watu hao walifumwa wakiwa tayari wameisha wachinja Ng’ombe hao na bila kuwachuna,waliwakata kata na kujaza nyama kwenye mifuko ya sadarusi.

“Walivamiwa na kuanza kupigwa kwa silaha za jadi na walipofariki dunia,walichomwa moto”,alisema.

Alisema uchunguzi ukikamilika,watu watakaobainika kuhusu na mauaji hayo ya kikatili,watafikishwa mahakamani kujibu tuhuma inayowakabili ya mauaji na wizi wa Ng’ombe.

“Kwa sasa hatuwezi kutangaza hadharani majina ya watuhumiwa tunaoendelea kuwashikilia, kwa vile kitendo hicho kinaweza kuharibu kazi ya upelelezi ambao bado unaendelea”, alisema kamanda Sedoyeka.

MH SITTA AMTETEA SHY ROSE BHANJI



Kumekuwa na taarifa kuhusu kuwepo migogoro mbalimbali inayohusisha Wabunge wawakilishi wa Tanzania katika Bunge la Afrika Mashariki ambapo Mbunge Shy-Rose Bhanji amehusishwa sana kwenye vichwa vya habari.

Kwenye kikao cha Bunge November 20 2014 Dodoma Hatibu ambae ni mbunge wa Zanzibar aliuliza ,"Sisi wabunge wa bunge hili ndiyo wapiga kura wa kuwachagua wawakilishi wetu wa kutuwakilisha katika bunge la Afrika Mashariki, kumekuwa na taarifa za kulipaka Taifa hili matope kulitia aibu kutokana na  baadhi ya wawakilishi wetu, Wabunge wetu wa Afrika Mashariki kutokana na matendo wanayoyafanya kule..”

“…Ni lini hasa kinachoendelea pale na hatua gani zilizochukuliwa kuhusu ukosefu wa nidhamu uliojitokeza kwa mbunge Shyrose Banji wazi wazi na ili hali hakuna taarifa yoyote, Mheshimiwa Naibu Spika naomba mwongozo wako…”– Hatibu.

Baada ya swali waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta akawasha kipaza sauti na kutoa haya majibu “…Naomba nitoe taarifa kwamba kinachotokea katika Bunge la Afrika Mashariki kwa kiasi kikubwa kinahusu mgogoro wa  spika mwenyewe, hilo ndiyo chanzo cha matatizo mengi, kwa hiyo  wabunge  wa Bunge la  Afrika Mashariki wamegawika kataka makundi mawili, kuna kundi linalotaka Spika lazma aondolewe, na wengine wanadai wanamtetea abaki…”
..Sasa katika kundi ambalo wanataka  abaki imeonekana Tanzania ndio kikwazo, kwa sababu ili upate uamuzi ndani la Bunge la Afrika Mashariki  katika suala lolote lazima upate akidi inayotosheleza kutoka  kila nchi, sasa wabunge wa Tanzania ambao mwanzoni waliunga mkono hoja ya kumuondoa yule Spika wamefuta hilo na wamekubaliana aendelee kwa hiyo imeleta chuku kiasi Fulani…“– Sitta.
 “…Katika tukio ambalo limetokea juzi nasema hivi kwa sababu  Naibu Waziri wangu yuko kule kwa hiyo ni jambo halisi, kilichotokea sio kama kinavyoelezwa Mheshimiwa Shyrose Banji ambaye anahesabika ni mfuasi mkubwa wa Yule Spika kiasi kwamba wenzie wanamuona kama kibaraka vile, alikuwa anapita katikati ya Wabunge wengine kuwahi usafiri kwa bahati mbaya akamgonga Mheshimiwa Ndelakindo Kessy, Mheshimiwa Ndelakindo akahamaki na kwa kusaidiwa na  baadhi ya Wabunge  wengine wa Uganda akaenda kituo cha Polisi kutoa taarifa kwa madai kwamba amefanyiwa makosa ya jinai wanaita ‘assaults’…“– Sitta.

Ikabidi aitwe ‘Sergeant at Arms’ wa Bunge la EALA ambaye alikwishaanza jitihada za kulifanya jambo lile liishie ndani ya Bunge na katika jitihada hizo alifika mbali kidogo akawezesha Wabunge wetu hao wawili waweze kusikilizana na ninavyotoa taarifa hivi sasa ni kwamba jana suala hili limekwisha na haliendelezwi na Polisi tena…
“– Sitta.Hivi ndivyo Waziri Sitta alimalizia kujibu suala hilo;

Sasa yale mengine yaliyosema kwamba alifanya mambo ya hovyo Mheshimiwa yule tena kama miezi miwili iliyopita, bado yako mikononi mwa tume ya Bunge la Afrika Mashariki hadi hapo watakapolishughulikia hatuwezi kufanya kitu chochote, na tukishapata taarifa ya tume ya Bunge la Afrika Mashariki basi mimi nitatoa taarifa kwa Mheshimiwa Spika ili sasa sisi kwa wote kama jimbo la uchaguzi La Wabunge hao tuone ukweli ni upi na tujue hatua ya kuchukua..”– Sitta.

MAGAZETI YA UDAKU NA MICHEZO










MAGAZETI YA KIBONGO LEO HII





8