Sunday 30 November 2014

HAPANA CHEZEA WACHINA...WAICOPY RANGE ROVER KAMA ILIVYOOOOOO NA KUUZA BEI CHEEEEEEE.......

   


 Hili Range Rover Evoque ambalo linauzwa Pound 40,000.   

Ukisikia Wachina balaa sasa hii ni moja wapo, Kiwanda Kimojawapo cha China kijulikanacho kwa jina la LandWind kimeibuka na Kutengeneza Range Rover Off-Roader  X7 na kuliuza kwa bei Chee kabisa Pound 14,000 ambalo Linafanana kila kitu na Range Rover Jipya kutoka Uingeleza Linalokwenda kwa Jina la Range Rover Off-Roader ambalo wao waingeleza wanaliuza kwa Pound 40,000 ambapo tofauti yake ni Kubwa sana. 
Swala hilo ambalo ni kinyume cha sheria litapelekea Kiwanda hicho kufunguliwa mashitaka kwa kosa hilo la kuiba ujuzi.
Kwa Mara ya kwanza wakati limeingia Dukani wapenzi wengi wa Magari walijua kabisa kuwa lile lilikuwa ni Range Rover evoque kutoka uingeleza ambalo ndilo 'Latest Model' kwa kuwa lilifanana kila kitu , lakini ukweli ni Kwamba Lilikuwa sio bali ni Copy yake tuu ambayo wachina walichakachua

 Sasa Hili ni Lile la kichina ambalo limezinduliwa wiki iliyopita na Kampuni ya Landwind huko Guangzhou Ni Range Rover X7 na Bei yake ni poa kabisa Pound 14,000 tuu
Je Mdau unaona kuna tofauti yoyote kati ya Magari hayo?

CHANZO: GAZETI LA THIS DAY

No comments: