Saturday 22 November 2014

BONDIA MTANZANIA NA MANNY PACQUAIO KUPANDA ULINGONI USIKU WA LEO


BONDIA wa Tanzania wa Ngumi za Kulipwa, Fadhil Majia usiku wa leo Jumamosi anatarajia kupanda ulingoni nchini China kuzichapa na Jerwin Ancajas katika pambano la utangulizi la kimataifa kati ya Mfilipino, Manny Pacquaio na Cris Ageiri.

Tanzania ndiyo nchi pekee kutoka Afrika yenye bondia katika pambano hilo kubwa duniani litakalofanyika kwenye Ukumbi wa Cotai Arena, Venetian Resort, Macao humo.Akizungumza na Championi Jumamosi, Katibu wa Shirikisho la Ngumi za Kulipwa Tanzania (PST), Anthoy Rutta, alisema Manny Pacquiao na Fadhili Majia wamepima uzito jana usiku tayari kwa pambano hilo.

“Mabondia wote watakaocheza kwenye pambano la Jumamosi (leo) wamepima uzito na afya zao usiku wa jana akiwemo Manny Pacquaio na Mtanzania Fadhil Majia tayari kwa kazi hiyo.

“Majia ndiye atakuwa bondia wa kwanza kucheza pambano la utangulizi na Jerwin Ancajas, pia ni bondia pekee anayetokea barani Afrika, hivyo tunamtakia kila la kheri katika pambano lake,” alisema Rutta.  
Source: Gazeti la Champion Jumamosi

No comments: