Friday 21 November 2014

PUTIN: MAREKANI NA WAPAMBE WAKE WAMECHEMKA


Rais Vladimir Putin wa Russia amesema kuwa juhudi za Marekani za kutaka kuipigisha magoti nchi yake zimegonga mwamba. Rais Putin amesema kuwa vikwazo vilivyowekwa na Marekani na waitifaki wake dhidi ya Russia ni fursa kwa ajili ya ustawi wa nchi hiyo. Putin amesema kuwa, nchi zilizoiwekea Russia vikwazo zina matatizo mbalimbali na kwamba zimepoteza masoko ya bidhaa za chakula na za kilimo ya Russia. Ameongeza kuwa na hapa ninamkuu" sisi tumestafidi na miamala mibaya ya washirika wetu na nchi ambazo zilikuwa zimepata nafasi katika masoko ya bidhaa za chakula na kilimo za Russia na tumeziwekea vikwazo nchi hizo" mwisho wa kunukuu.

Rais wa Russia amesisitiza pia juu ya udharura wa kustafidi na sekta za kiuchumi za Russia zinazotokana na fursa zilizopotea kutokana na vikwazo vya nchi za Magharibi na Moscow kujibu vikwazo hivyo sambamba na kuboresha uwezo wake katika nyanja mbalimbali za nchi hiyo.

No comments: