Thursday 20 November 2014

SERIKALI KUTUMIA BILIONI 20 UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA


Serikali imesema kuwa itatumia bilioni20 kwa ajili ya uchaguzi wa Serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika December14 mwaka huu.
Mkurugenzi wa Idara ya Serikali za Mitaa Ofisi ya Waziri mkuu (Tamisemi) Kharist Luhanda alisema jana kuwa gharama hizo zitajumuisha tangu kuanza kwa zoezi zima la maandalizi ya uchaguzi huo mpaka siku ya upigaji kura utakapokamilika.
Alisema gharama nyingine ni kwa ajili ya kusafirisha masanduku,kulipa posho kwa watakaohusika na usimamizi wa uchaguzi,usafiri,kulipa wasimamizi wa uchaguzi na semina mbalimbali zilizokuwa zikitolewa kwa ajili ya elimu.

No comments: