Friday 21 November 2014

HALI MBAYA YA KIBINADAM YANUKIA LIBYA


Kamisheni ya taifa ya kutetea haki za binadamu nchini Libya imetahadharisha juu ya uwezekano wa kuzuka hali mbaya ya kibinadamu katika nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika. Taarifa ya kamisheni hiyo imesema kuwa, kutokana na kushitadi ghasia na machafuko, idadi ya wakimbizi wa ndani na nje ya nchi inazidi kuongezeka kila uchao; jambo linaloweza kusababisha kuibuka hali mbaya ya kibinadamu. Kwa mujibu wa ripoti hiyo, tayari idadi ya wakimbizi kwenye kambi za ndani ya nchi imeongezeka katika hali ambayo huduma muhimu kama vile maji na vyoo ni adimu.

Mapigano kati ya jeshi la serikali na makundi ya wanamgambo wenye silaha nchini Libya hadi sasa yamesababisha zaidi ya watu nusu milioni kukimbia makazi yao na kuwa wakimbizi ndani ya nchi huku wengine wengi wakikimbilia nchi jirani za Misri na Tunisia kutafuta hifadhi. 

No comments: