Friday 21 November 2014

BOKO HARAM YAUA 45 NIGERIA


Shambulizi linalodhaniwa kuwa la wapiganaji wa kundi la kitakfiri la Boko Haram limeua watu wasiopungua 45 huko kaskazini mashariki mwa Nigeria.
Shambulizi hilo limefanyika katika kijiji cha Azaya Kura katika eneo la Mafa kwenye jimbo la Borno na baadhi ya walioshuhudia tukio hilo wanasema idadi ya watu waliouawa huwenda ikaongezeka kutokana na majeruhi wengi wa shambulizi hilo.
Kaimu wa Gavana wa jimbo hilo Shettima Lawan ameiomba serikali kuu ya Nigeria kuchukua hatua za haraka za kuwaokoa watu wa eneo hilo.
Shambulizi hilo limefanyika siku chache baada ya Waziri wa Sheria wa Nigeria Mohammed Adoke kusema kuwa, Rais Goodluck Jonathan wa nchi hiyo anatarajiwa kuliomba Bunge lirefushe muda wa hali ya hatari katika majimbo ya Yobe, Borno na Adamawa kutokana na machafuko yanayosababishwa na kundi la Boko haram.
Kundi hilo linahusika na mashambulizi na mauaji mengi yanayofanyika katika maeneo hayo ya kaskazini mwa Nigeria.

No comments: