Wednesday 26 November 2014

BOKO HARAM WAENDELEA KUFANYA YAO....SASA WATEKA MJI MWINGINEMWINGINE WA KASKAZIN

Duru za habari nchini Nigeria, zimetangaza kuwa, wanamgambo wa kundi la kigaidi na kitakfiri wa Boko Haram wameudhibiti mji mwengine wa kaskazini mashariki mwa nchi hiyo. Hayo yamethibitishwa leo na kiongozi mmoja wa serikali katika bunge la seneti nchini Nigeria ambaye ni mkazi wa jimbo la Borno na kuongeza kuwa, wanachama wa kundi hilo lenye uelewa potofu kuhusu mafundisho ya Uislamu, wameudhibiti mji wa mpakani wa Damasak. Seneta huyo ameongeza kuwa, hivi sasa mji huo umetwaliwa na kundi hilo na kwamba, raia na askari wamelazimika kukimbia kuokoa maisha yao. Inaelezwa kuwa, awali wanamgambo wa kundi hilo waliokuwa wameficha silaha zao katika magari aina ya malori, walipeleka magari hayo katika soko la mji huo, na kuanza kuwamiminia risasi wafanyabiashara na raia wa kawaida, ambapo makumi ya watu waliuawa. Seneta huyo ameongeza kuwa, baada ya wanachama wa kundi hilo la Boko Haram kuudhibiti mji huo, walianza kubomoa na kuharibu nyumba nyingi ikiwemo hospitali na kwamba hadi sasa makumi ya wasichana na watoto wadogo wametekwa na magaidi hao.

No comments: