Tuesday 25 November 2014

WAZIRI WA ULINZI WA MAREKANI,CHURK HAGEL,HAJIULIZI


Habari kutoka Pentagon zinasema kuwa, Hagel amekuwa akifanya mazungumzo na Rais Barack Obama tangu mwezi Oktoba kuhusu kujiuzulu kwake. Duru za ndani ya Pentagon zinasema Rais Obama alimuomba Hagel kujiuzulu baada ya chama chake cha Democrats kushindwa vibaya kwenye uchaguzi mdogo uliokamilika majuzi. Imedaiwa kuwa, Hagel ameshindwa kukabiliana na changamoto za hivi karibuni zinazolikabili jeshi la Marekani ikiwemo kadhia ya Afghanistan na oparesheni dhidi ya kundi la kigaidi la ISIL. Hagel ataendelea kushikilia wadhifa wake hadi papatikane shaksia mwingine wa kujaza nafasi hiyo.

Jack Reed, Seneta wa jimbo la Rhode Island ni miongoni mwa wale wanaopigiwa upatu wa kuchukua nafasi hiyo.

No comments: