Friday 28 November 2014

MH.KANGI LUGOLA AVAA KININJA BUNGENI ILI ASIWATAZAME WAHUSIKA WA SAKATA LA ESCROW



MBUNGE wa Mwibara (CCM), Alphaxard Kangi Lugola wakati akichangia katika Ripoti ya PAC kuhusu sakata la Akaunti ya Tegeta Escrow bungeni leo, ameomba kuchangia huku akiwa amevaa 'Kininja' ili kutowaangalia usoni wahusika wa sakata hilo.
 
Mbali na kuvaa hivyo, Lugola pia aliomba kama kanuni zinaruhusu achangie tena akiwa amevaa nguo za chama chake cha CCM ili kuonyesha kuwa CCM haiungi mkono vitendo viovu japo alikataliwa na Mwenyekiti wa Bunge, Mhe. Zungu.

No comments: