Thursday 27 November 2014

Mh MKONO HAKULISHWA SUMU


         Mh.Nimrod Mkono (MB).

Siku chache baada ya Mbunge wa Musoma vijijini Nimrodi Mkono kusema amelishwa sumu akiwa London Uingereza,Mbunge wa Chadema Halima Mdee amemtaka kusema ukweli na si kulihadaa Taifa kwa uongo.
Mkono alisema leng la kulishwa sumu ni kutaka kuharibu figo zake ndani ya saa72 lakini kitendo hicho kilichoshindikana.
Mdee aliyekua na Mkono katika ziara hiyo nchini Uingereza alisema hakuna ukweli wowote kuhusu yeye kutaka kulishwa sumu,nilikua naye kule na mazingira ya kuanza kuumwa hadi kupona kwake ni utata mtupu….awaeleze Watanzania anaumwa nini na si kusingizia alilishwa sumu,”alisema.
‘Kama anataka kutumia kivuli cha Escrow,arudi bungeni tuweze kujadili na tuimalize ili asiseme kuwa sijui wanataka kumuua ni uongo.

No comments: