Saturday 29 November 2014

BARUA YA WAZI KWA WEMA SEPETU



Najua wewe ni mrembo sana ,una exposure na unapesa.sawa wanasema mwanamke bila mwanaume haiwezekani ila kwa mimi naona inawezekana jana nimekuona sehemu fulani kinondoni umelewa sana sana...hivi unadhani pombe ndio suruhisho la matatizo yako? tena unakunywa mi pombe mikali halafu wewe mwanamke .iko kizazi kitapona kweli kwa staili hiyo? nikupe siri mdogo wangu wewe ni mzuri sana una nafasi ya kuwa na mwanaume yeyote dunia hii na sio uchafu wa manzese huu unaokupaka paka vikwapa vya kila mwanamke .. kama ungeweza embu ondoka tanzania japo kwa miezi 6 nenda kakae zako nje ya nchi kama ulivyofanya kipindi kile ulipoachana na yule mla unga ..ukirudi utakuwa mpya wema mpya utakuwa umeweza kukaa mbali na huyo domo na utaona unaweza kuishi bila yeye 3.embu jaribu kukaa bila mwanaume uone kama haiwezekaniki.. jaribu kubadiri aina ya wanaume unao date .date watu wa nje ya nchi uone kama yatajirudia haya haya au utaendelea kuvaa sare za harusi za wenzio huku pete ulovalishwa mwaka arubaini na saba ikiotea kutu kidoleni mwako imefika stage watu wanaona wewe kigodoro cha kukimbilia pale magodoro yao yanapoingia kunguni .. wafungie vioo hao fanya yako.. anzisha kitu cha kuku keep busy acha pombe , ikiwezekana hata zile company za kunywa zikimbie.. wewe ni mdogo sanasana kunywa mi pombe ati stress za mapenzi utajipatia maradhi ya figo ungali mdogo labda kama mwenzetu wataka kufa kesho tuambie ili tukuwekee oda ya mi dompo mia kila siku nasisitiza sana jaribu kubadiri aina ya wanaume unaotoka nao .acha waume za watu nenda nje ya nchi jipatie mkaka au mzungu kama dadako alivofanyaga .katulia date mtu wa mbali na kwenu wa hapa kwenu hakuna wa kukuoa woote watakutumia kujipatia majina hawakupendi wemaa.. wanataka u star kupitia wewe... ona wenzio ma miss wamesha tengeneza familia zao .. wewe bado huolewi na umri una songa ..na kibaya zaidi mdogo wangu una mwili mbaya wa kuzeeka haraka na hio mi pombe ndo kabisaa..najui inaumiza hii ila ukija sikia utakubali....

No comments: