Sunday 14 December 2014

MSANII BONGO MUVI ATAKA KUJIUA KISA YANGA KUCHAPWA NA SIMBA.....

Baada ya Simba kumshushia kipigo kikali Yanga  cha mabao mawili kwa sifuri, nakuibuka mtani jembe. Muigizaji na shabiki mkubwa wa timu ya Yanga, Mchopanga  inasemekana alitaka kumeza madawa baada ya kuchapa kilaji. 


Ripoti kutoka kwa JB, ambae ni shabiki kindakindaki wa timu ya Simba.
“Tahadhari: unaweza ukadharau lakini nikweli.tulitumia zaidi ya masaa2 kumtuliza chopa asimeze madawa.kwanza alianza kulewa uwanjani mara tu baada ya goli la pili.alikuwa analia muda wote.kisha akajifungia.tulifanikiwa kupata funguo za ziada na tulipofungua tulimkuta kama kachanganyikiwa.angalia macho yake.kama una ndugu yako ni yanga usimwache. peke yake ni hatari daah watajiua hawa.”


No comments: