Thursday 11 December 2014

YUSUPH MLELA AKANA KUTUMIA UNGA

 


MSANII anayefanya vizuri katika filamu Bongo, Yusuf Mlela ambaye amekuwa akidaiwa kutumia madawa ya kulevya maarufu kama unga, amesema utofauti wa muonekano wake kwa sasa siyo kwa sababu ya uteja, bali inatokana na umri wake kusogea.

“Unajua mtu unavyozidi kukua na muonekano nao unabadilika, lakini itafikia kipindi nitakuwa sawa tu hivyo naomba mashabiki wangu waelewe kwamba mimi siyo teja na sijawahi kutumia ‘unga’ hizo ni habari za kizushi tu,”alisema Mlela.
Hivi karibuni Mlela alitupia picha kwenye mtandao wa Instagram ambapo wadau mbalimbali walionekana kushangazwa na muonekano wake na kumfananisha na mateja.

No comments: