Friday 12 December 2014

TABIA YA KUGOMBANIA MABWANA,DIDA AFUNGUKA ......




Mtangazaji wa Redio Times FM, Khadija Shaibu ‘Dida’ akipozi.

MTANGAZAJI wa Redio Times FM, Khadija Shaibu ‘Dida’ amesema siku zote anapokuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi akigundua mtu wake ana ‘date’ na mwanamke mwingine, kamwe hatathubutu kugombea bwana ila atanawa mikono
Akibonga na paparazi wetu hivi karibuni Dida alisema, hakuna kitu ambacho kwake anaona ni cha kipuuzi kama kugombea penzi, kwa kuwa mtu anapokusaliti ni wazi upendo wake umehamia kwa mtu mwingine hivyo hawezi kujing’ang’aniza. 
“Nawashangaa sana wasichana wanaokosa kazi ya kufanya kwa kuanza kuwagombea wanaume, wengine wanadundana hadi kutoana manundu, hivi nigombee bwana kwani wanaume wameisha? Mimi nikimkuta mtu wangu yupo na mtu mwingine wala sijishughulishi, nachukua hamsini zangu,” alisema Dida.

No comments: