Wednesday 21 January 2015

AUNTY EZEKIEL AMSHANGAA KING MAJUTO KUKATAA KUSHIRIKISHWA KWENYE FILAMU ZA WASANII WENZAKE

                                          
Msanii wa filamu Bongo, Aunty Ezekiel.
WAKATI mkongwe wa filamu za kuchekesha, King Majuto akidai kutoshiriki kazi na msanii yeyote kutokana na kuibiwa, msanii mwenzake, Aunty Ezekiel amechukizwa na uamuzi huo.Akizungumza na Uwazi, Aunty alisema kuwa haamini kama wezi wa kazi zake ndiyo chanzo cha Majuto kuachana na filamu za kushirikishwa bali inawezekana kuna tatizo lake lingine.


Mkongwe wa filamu za kuchekesha, King Majuto.
“Suala la wezi lipo miaka mingi na kama mkongwe na mpenda maendeleo alitakiwa kusimama maana kila mmoja akisema achukue uamuzi kama huo ni wazi kwamba kutakuwa hakuna msanii tena Tanzania,” alisema.

No comments: