Monday 19 January 2015

SIR NATURE KUGOMBEA UBUNGE TEMEKE

                           

Msanii nguli wa kizazi kipya Juma Kasim kiroboto almaarufu Sir Nature ametangaza rasmi nia ya kugombea ubunge jimbo la temeke.  


Pamoja na kutangaza huko nia yake hiyo,sir Nature alishindwa kuweka bayana ni chama gani atatumia kutimiza lengo hilo la kutaka kuwawakilisha wakazi wa jimbo la Temeke katika bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania.

Tetesi zinanyetisha kuwa awali ilikuwa atangaze nia kupitia chama cha wananchi CUF,lakini mbunge wa Mbeya mjini kupitia tiketi ya Chadema mh Joseph Mbilinyi Sugu alimshauri kugombea kupitia Chadema jambo ambalo bado analifikiria. 

No comments: