Friday 23 January 2015

MASOGANGE ATUHUMIWA KUTUMIA INSTAGRAM KUJIUZA HUKO SAUZI

     
MIEZI michache tangu ahamishie makazi yake nchini Afrika Kusini, modo aliyetikisa Bongo, Agnes Gerald ‘Masogange’ ametia aibu kutokana na kudaiwa ‘kujiuza’ kwa njia ya mtandao nchini humo. 


Modo anayetikisa Bongo, Agnes Gerald ‘Masogange’. 
Chanzo makini kilicho karibu na staa huyo kimepenyeza ubuyu kuwa, Masogange yupoyupo tu, kazi kujipiga picha za utupu na kuzitupia mtandaoni kana kwamba anatafuta wanaume.“Kimsingi hana kazi huku Sauz zaidi ya kuposti picha kwenye mtandao wa Instagram na anachanganya sana wanaume wenye pesa zao, si unajua tena mtoto kajaliwa shepu la maana.
“Ukitaka kuthibitisha hilo ninalokwambia, ingia katika akaunti yake utaona picha kibao za kihasara akiwa hotelini, kama siyo kutuaibisha na kujiaibisha mwenyewe ni nini?” kilihoji chanzo chetu. 
Agnes Gerald ‘Masogange’ akipozi. 

Baada ya chanzo hicho kuvujisha ubuyu huo, paparazi wetu aliingia kwenye akaunti ya mrembo huyo na kujionea picha kibao zenye mapozi ya kihasara. Jitihada za kumpata ili azungumzie madai hayo hazikuzaa matunda kwani simu yake haikuwa hewani lakini katika maelezo yake kwenye mitandao ya kijamii amewahi kudai anasoma chuo ingawa haijajulikana ni chuo gani. 
 
CHANZO:GAZETI LA IJUMAA



No comments: