Thursday 27 November 2014

ESCROW NDO MPANGO WA MJINI



RUTI MPYAAAAAAAAA...
KITU CHA T/ESCROW KKOO NAULI 400 KAMA KAWA

MTATIRO: NCHI IMEOZA HADI ALTARENI

                              Askofu Kilaini

HII NI KAULI ALIYOITOA JULIUS MTATIRO BAADA YA VIONGOZI WA DINI KUWA KWENYE LIST YA WALIOPATA MGAWO WA MABILIONI YA ESCROW
Tunapokuwa na nchi iliyooza, viongozi wa dini wako mstari wa mbele kuchukua milungula na hela za rushwa zilizojaa damu na mateso ya kodi za wananchi.Ni aibu mno, sielewi hawa maaskofu wangu wanasimama kwenye altare kufanya nini...ni kufuru na aibu kwa mimi Mkatoliki na wakatoliki wote duniani.
Wakati Bunge linafukuza wezi, ni muhimu na Kanisa Katoliki lifukuze hawa maaskofu walafi na kuwapeleka mahakamani. Kisha kanisa lijivue ushenzi huu, lirejeshe pesa hizi kwa niaba ya watumishi hawa walafi wa fedha na mafisadi.
Shame on you beloved bishops, my bishops... 
#BishopMethodius #Kilaini & #BishopEusebius #Nzingilwa. 
#IPTL & #ESCROW #BringBackOurMoney.

SHILOLE TOTO LA KINYAMWEZI LATUA UBELGIJI....CHEKI MAFOTO YAKE HAPA ALIVYOPOKELEWA...










BREKI ZA NDEGE ZAGANDA BAADA YA KUPIGWA NA BARIDI KALI


Abiria waliokuwa wanafanya safari na shirika la ndege la Serbia walilazimika kushuka katika ndege hiyo na kuisukuma baada ya breki zake kuganda na kushindwa kuondoka.
Ndege hiyo ilikuwa inaanza kuruka kutoka katika mji wa Kirusi wa Igarka,lakini ilishindwa kusogea baada ya hali ya hewa kuwa -52C.
Abiria waliokuwa ndani ya ndege hiyo idadi yao kubwa walikuwa wafanyakazi wa ndege hiyo waliombwa kutoa msaada wa dharura wa kuisukuma ndege hiyo kwa hofu ya kutowachelewesha endapo watasubiri msaada Zaidi.
Ndege hiyo ya shirika la ndege la Katekavia baada ya muda ilimudu kuendelea na safari zake na baadaye kutua salama katika mji wa Krasnoyarsk.kwa muujibu wa mashuhuda wa tukio hili kiwango cha baridikwa muujibu wa mashuhuda wa tukio hili ,wanaeleza kuwa kiwango cha baridi kilishuka hadi kufikia nyuzi joto 52, na kugandisha mfumo wa breki za ndege hiyo .
Mkuu wa kitengo cha huduma za ndege hiyo Oxana Gorbunova, anaeleza kwama abiria hawakulazimishwa kuisukuma ndege hiyo bali kwa hiyari waliamua kusaidia kuisukuma ,japokuwa kitendo hicho hakiruhusiwi kwakuwa kitendo hicho kinaweza kuathiri bodi ya nje ya ndege hiyo ,na wanasheria nao wanachunguza endapo uwanja wa ndege,shirika la ndege,wafanyakazi wa ndege ama abiria endapo wamevunja sheria za usalama wa anga.
Uwanja huo wa ndege unatumiwa na abiria takribani elfu moja kwa mwaka ,wengi wao hufanya kazi katika makampuni ya mafuta yanayomilikiwa na Urusi.
CHANZO:BBC

MAMA MJAMZITO AMPIGA TAFU MUMEWE KUBAKA BINTI WA MIAKA 7


Mwanamke mmoja nchini China ambaye ni mjamzito amehukumiwa kifungo cha maisha huku mume wake akihukumiwa adhabu ya kifo baada ya kushirikiana kumbaka na kisha kumuua msichana wa miaka17.
Mwanamke huyo ambaye anajulikana kwa jina la Tan Beibei alifanya kitendo hicho baada ya msichana huyo kumsaidia alipoanguka barabarani ambapo alimpeleka hadi nyumbani kwake na badala ya kumshukuru waliamua kumfanyia kitendo hicho cha akishirikiana na mumewe kisha kumuua na kuamua kumzika.
Mahakama ya Heillojiang ya nchini humo imesema kuwa imewafungulia mashtaka ya kuua,kubaka pamoja na kushambulia baada ya mwanamke huyo kujifanya ni mgonjwa na kushirikiana na mumewe kumfanyia binti huyo kitendo hicho cha kudhalilisha kisa wivu kwa madai alikua akitembea na mumewe.
Mahakama ya juu ilikataa kuwapunguzia adhabu wawili hao baada ya kukata rufaa kwa madai kesi hiyo ni kubwa na haina dhamana yoyote.
Kwa mujibu wa mashuhuda msichana huyo aliyejulikana kwa jina la Hu alikua akipita barabarani ndipo mama huyo alipomwomba msaada wa kumpeleka nyumbani kwake baada ya kuanguka na msichana huyo kutii lakini alipofika alikutana na maswaiba hayo.
Inaelezwa kuwa baada ya kufika mume wa mwanamke huyo alimpa msichana huyo maziwa ya mtindi na baadaye kuanza kumfanya kitendo hicho lakini hata hivyo hawakufanikiwa kwani binti huyo aliweza kuwazidi nguvu na walipoona imeshindikana walichukua blanketi na kumziba nalo usoni hadi alipofariki dunia na kuamua kumzika.
Katika utetezi wa mwanamke huyo mahakamani hapo alisema aliamua kufanya kitendo hicho kwa sababu binti huyo alikua akitembea na mume wake.
Historia inaonyesha wawili hao walishawahi kuwa na kesi mbalimbali kiwemo ya kutaka kumbaka rafiki wa mtoto wao wa kike ambaye alikua akisoma naye darasa moja.

BAADA YA KIM KARDASHIAN SASA NI ZAMU YA WIZ KHALIFA KAJIFOTOA MTUPUUUUUUU AKIWA BAFUNI


Ikiwa zimepita siku kadhaa tangu Supastaa Kim Kadarshian kukaa kwenye vichwa vya habari vya mitandao mbalimbali kutokana na picha zake zikimuonyesha akiwa tupu kuzagaa kwenye mitandao, staa mwingine tena huenda akaingia kwenye list ya #BreaktheInternet.
Kwenye ukurasa wa Rapa Wiz Khalifa ameweka picha inayomwonyesha akijimwagia maji kichwani huku akiwa mtupu ndani ya bafu.
Bado haijafahamika kama amefanya hivyo kama njia ya kuyatangaza maji hayo au ana maana ipi.

KASHFA YA MISS TANZANIA 2014,UTATA MPYAAAAAAA WAIBUKA


Hatima ya kashfa ya kudanganya umri inayomkabili aliyekuwa mrembo wa Tanzania mwaka 2014, Sitti Mtemvu bado ipo kizani baada ya polisi kuikana kauli ya Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (Rita).

Rita, kwa upande wao ilieleza wiki moja iliyopita kuwa imekabidhi polisi vielelezo kuhusu uchunguzi wa kashfa hiyo kwa lengo la kuchukua hatua.

Juzi, Kamishna wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova alikana kupokea taarifa za vielelezo hivyo vilivyotumiwa kuombea cheti cha kuzaliwa cha Sitti Mtemvu.

Wiki mbili zilizopita, Wizara ya Habari, Utamaduni, Vijana na Michezo kupitia Baraza la Sanaa la Taifa (Basata) ilijivua lawama katika kashfa hiyo na kuiachia Rita.

Akizungumza na gazeti hili juzi, Kova alisema, “Jeshi la Polisi halijapokea vielelezo vyovyote kutoka Rita, wamepeleka wapi? Iwapo waliviwasilisha katika kituo chochote cha polisi watoe taarifa iliyo sahihi, iwapo vielelezo hivyo vitatufikia tutachukua hatua stahiki,” alisema Kova.

Kwa upande wao, Rita waliahidi kuwasilisha vielelezo hivyo wiki hii na kwamba vilicheleweshwa kutokana na kukamilisha upekuzi wa taarifa za kuombea cheti pamoja na cheti cha awali kilichokuwa kikitumiwa na Sitti Mtemvu.

Mkurugenzi wa Idara ya Sheria wa Rita, Emmy Harrison alisema jana kuwa idara yake imekamilisha taratibu zote zinazotakiwa na vielelezo hivyo vitakabidhiwa rasmi polisi.

“Haya ni masuala ya kisheria, hivyo sisi tumeshakamilisha kile tulichotakiwa kukifanya na mchakato huu bado unaendelea, tupo katika maandalizi ya mwisho kwa ajili ya kuripoti polisi, wiki hii vielelezo vya Sitti vitapelekwa kwenye vyombo vya usalama kwa ajili ya hatua zaidi,” alisema Harrison.
CHANZO: MWANANCHI

MRITHI WA JAJA HUYOOOOOOOOO KASHATUA.......



Nyota mpya wa Klabu ya soka ya Yanga ya Dar es Salaam, anayekuja kufanya majaribio ya kuziba nafasi ya Mbrazil mwenzake Genlson Santos 'Jaja', Emerson De Oliveria Neves Rouqe akitoa ishara ya dole mara baada ya kuwasili uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere (JNIA) Dar es Salaam na kupokelewa na viongozi wa Yanga. 
Rouque aliwasili na Kocha mkuu wa Yanga, Marcio Maximo pamoja na Nyota mwingine kutoka Brazili Andrew Coutinho.