Monday 19 January 2015

RONALDO (CR7) AACHANA NA MPENZI WAKE WA SIKU NYINGI

         

SIRI imefichuka!. Cristiano Ronaldo alisherehekea mwaka mpya peke yake baada ya mchumba wake, Mrusi kutokwenda katika sherehe ya siri aliyoandaa nyumbani kwao Madeira, gazeti maarufu la Ureno la Correio da Manha rimeripoti. 
Gazeti hilo limetoa habari jana na kuthibitisha kuwa familia ya Ronaldo imevunjika baada kukosekana kwa maelewano baina ya Ronaldo na mpenzi wake Irina. 

MWIZI WA AKAUNTI ZA AY NA FID Q HUYU HAPA,NI MTOTO WA MBUNGE...

                                             
Ahmed Mundhiri, kumbe ni mtoto wa Mbunge wa zamani wa Mchinga Mh. Mdhihiri Mdhihiri amekamatwa jana kwa kuiba account za watu mbali mbali kwenye mitandao wakiwemo Fid Q na AY kama anavyoonekana aliponaswa jana live!!

SIR NATURE KUGOMBEA UBUNGE TEMEKE

                           

Msanii nguli wa kizazi kipya Juma Kasim kiroboto almaarufu Sir Nature ametangaza rasmi nia ya kugombea ubunge jimbo la temeke.  

Sunday 18 January 2015

MCHUNGAJI MTIKILA AMSHTAKI ASKOFU MOKIWA BAADA YA KUMSHIKA MAKALIO ADAI FIDIA YA BILIONI MOJA


Mchungaji Christopher Mtikila amefungua kesi katika mahakama ya hakimu mkazi Kisutu kumshitaki Askofu Mkuu wa Kanisa la Anglican Tanzania Dk. Valentino Mokiwa.
Msingi wa kesi ni kwamba Askofu Mokiwa alimshika makalio Mtikila na kwamba kitendo hicho kilichotokea Juni 25 mwaka jana walipokutana maeneo ya Ilala, kimemdhalilisha.
Mtikila alikuwa ameitwa na Askofu kujadili tamko la la Mtikila kwamba Kanisa la Anglican linajihusisha na ufisadi, ukiwemo wizi wa vifaa vya Hospitali ya Mission ya Millo iliyoko Ludewa mkoani Njombe. 

DIAMOND NA KIBA WAKUTANA UKUMBINI,WACHUNIANA....

     
Kama ulikuwa unaamini kuwa lile bifu la wakali wawili wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ na Ali Saleh Kiba, limekwisha, basi utakuwa utakuwa unakosea na kujidanganya vibaya mnooooo.....Bifu bado lipo na hii imegundulika baada ya jamaa hao kukutana ukumbini na kuchuniana. 

LULU: SICHANGANYI MADAWA KAMA WENGINE,NITABAKI KUWA MUIGIZA


MTOTO mzuri Bongo Movies, Elizabeth Michael ‘Lulu’ amesema katika maisha yake ya sanaa hataweza kuchanganya madawa kufanya kazi nyingine mbali na kuigiza kama ambavyo wasanii wengine wanafanya. 

AMINI USIAMINI,MJI WA DUBAI UNAONGOZA KWA UAMINIFU SOMA TAARIFA HII...

Dubai imejinyakulia sifa ya kipekee katika kupima Imani za jamii kwa pochi iliyoangushwa mtaani,na mara ikarejeshwa kwa mhusika mara moja. 

Katika utafiti uliofanywa na mtengeneza Filamu mwenye asili ya Uingereza katika mitaa ya Dubai, alijaribu mara arobaini na tano kuidondosha kwa makusudi na katika kila tukio msamaria aliyeiokota aliirejesha pochi hiyo kwa mmiliki wake. 

SALUNI INAYOTOA HUDUMA YA NGONO YAGUNDULIKA KINONDONI,WADADA WA KISOMALI NDIO WAHUDUMU,BEI NI TSHS 60,000 KWA TENDO..

 
Wakati suala la ajira likiwa bado ni kitendawili kikubwa kwa serikali, Jiji la Dar hivi sasa linatisha, baada ya watu kubuni mtindo mpya wa kujipatia fedha kwa kujihusisha na biashara haramu ya ngono katika maeneo yanayotambulika kufanya shughuli nyingine halali.