Wednesday 17 December 2014

TETESI:BARAZA JIPYA LA MAWAZIRI HILI HAPA...


Katika hali ambayo haikutarajiwa, rais Kikwete amefanya mabadiliko makubwa katika baraza lake la mawaziri. Mabadiliko hayo ambayo yatatangazwa leo jioni yamewatupilia mbali watuhumiwa wa ufisadi sambamba na wazembe katika utendaji. 

Waliotupwa nje kutokana na tuhumua za ufisadi ni pamoja na Anna Tibaijuka- aliyekuwa waziri wa ardhi nyumba na makazi, Sospeter Muhongo-aliyekuwa waziri wa nishati na madini huku Lazaro Nyalandu akihamishwa kutoka wizara ya mali asili na italii aliyokuwa akihudumu. 

Walioondolewa kwenye wizara zao za awali na kuhamishwa ni pamoja na Lazaro Nyalandu ambaye anarudi mazingira. Saada Mkuya Salum kutoka fedha na kuhamishiwa ikulu pamoja na Gaudensia Kabaka.Hayo ni baadhi ya majina niliyopata. 

UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA: AFUKUZWA BAADA YA KUMSHINDA BABA MWENYE NYUMBA


VITUKO vinazidi kuripotiwa katika chaguzi za serikali za mitaa zinazoendelea nchini na mjini Morogoro, mgombea kutoka muungano wa Ukawa, Sharrif Abdul Mnola (Chadema) ametimuliwa kwenye nyumba aliyokuwa anaishi baada ya kumshinda mpinzani wake, Makalla Salum Hassan (CCM) ambaye ni mmiliki wa mjengo huo uliopo mtaa wa Ngoma ‘A’ kata ya Mji Mpya.
Sharrif ambaye ni dalali wa magari alishinda baada ya kupata kura 79 huku Makalla akipata 72. 

MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI AJIUZURU..SOMA SABABU ALIYOTOA..


         
Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema amejiuzulu nafasi yake hiyo kuanzia jana,Jumanne, Desemba 16, 2014 na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amekubali ombi hilo la kujiuzulu.

Katika barua yake kwa Mhe. Rais Kikwete, Jaji Werema amesema kuwa ameomba kujiuzulu kwa sababu ushauri wake kuhusiana na suala ya Akaunti ya Tegeta Escrow hakueleweka na umechafua hali ya hewa.
Mhe. Rais Kikwete amemshukuru Jaji Werema kwa utumishi wake ulioongozwa na uaminifu na uadilifu.

Tuesday 16 December 2014

MAISHA HAYANA KANUNI...JOHARI AAMUA KUWA MUUZA NDIZI..MWENYEWE AFUNGUKA..


     
Muigizaji mkongwe wa filamu, Blandina Chagula ‘Johari’ amabae pia ni mkurugezi wa kampuni ya RJ ambayo inajihusisha na utengenezaji wa filamu hapa nchini.

MTUHUMIWA WA WIZI WA PIKIPIKI ANUSURIKA KUUAWA MAGOMENI LEO HII....


                                   


 KIJANA ambaye jina lake haikufahamika mara moja, amenusurika kuuawa na wananchi wenye hasira kwa tuhuma za wizi wa pikipiki jijini Dar.Tukio hilo la kusisimua limetokea asubuhi ya leo Magomeni-Mwembechai, ambapo lilisababisha foleni ndefu ya magari wakati kijana huyo akiadhibiwa na wananchi.

MISS TANZANIA HATARINI KUSITISHWA....

Hatma iwapo mashindano ya Miss Tanzania yataendelea au yatasitishwa kwa muda, itategemea majibu ya tathmini iliyofanyika mwishoni mwa wiki jana yanayotarajiwa kutolewa na Baraza la Sanaa la Taifa (Basata) wiki chache zijazo.  

DIAMOND ASINDIKIZWA NA MAGARI YA POLISI KWENDA AIRPORT HUKO MOMBASA

Diamond akisindikizwa Airport  Kwa Msafara wa Polisi Huko Mombasa 

YULE HOUSEGIRL WA UGANDA ALIEMTESA MTOTO AHUKUMIWA KWENDA JELA MIAKA 4

Jolly Tumuhirwe apatikana na hatia ya kumtesa mtoto mdogo na kufungwa jela miaka 4
Yaya wa Uganda aliyejipata pabaya kwa kumchapa mtoto wa mwajiri wake, amehukumiwa jela miaka minne kwa kosa la kumtesa mtoto.