Kocha wa Real Madrid, Muitaliano Carlo Ancelotti ameelezea uwepo wa Cristiano Ronaldo’s katika kikosi chake kama faida baada ya nyota huyo kufunga goli tatu peke yake (Hat-trick) na kufikisha jumla ya goli 200 katika kigi hiyo wakati madrid ilipoishindilia Celta Vigo 3-0.Katika pambano hilo, nyota huyo toka ureno, Cristiano Ronaldo alifunga goli zote tatu na hivyo kuvunja rekod ya hattrick ya la liga akifikisha 23, moja zaidi ya Magwiji Alfred Di Stefano na Telmo Zarra, huku zikiwa tatu zaidi ya mpinzani wake wa karibu Lionel Messi mwenye 20. Ikumbukwe nyota huyo sasa amefikisha jumla ya goli 200 katika michezo 178 pekee ya La Liga aliyoshiriki ikiwa ni kasi zaidi ya nyota yeyote.
Monday 8 December 2014
Subscribe to:
Posts (Atom)