Friday 5 December 2014
ZITTO KABWE KURUDI CHADEMA ATOA SHARTI MOJA TU...
Harufu ya kuisha kwa mgogoro baina ya Zitto Kabwe na chama chake cha Chadema inanukia, lakini mbunge huyo wa Kigoma Kaskazini anataka kuwapo na mazungumzo kubaini tatizo ili atakayebainika kuwa alifanya makosa awe tayari kuomba radhi hadharani.
MAMA WA KAMBO ALIYEMCHINJA MTOTO HUKO MARA NAE ACHINJWA.....
Tukio lilitokea hivi karibuni mkoani Mara la mama wa kambo kumchinja mtoto wake kwa kutumia panga hadi kufariki, limechukua sura mpya baada ya mama huyo nae kushambuliwa na wananchi wenye hasira kali kwa kukatwa katwa na mapanga mpaka kufariki.
Tukio la kukatwa katwa mapanga mama huyo limetokea baada ya wananchi wa kijijini hapo walioshikwa na jazba kali kwa kutokubaliana na kitendo cha kinyama alichomfanyia mtoto huyo kwa kumkatishia maisha yake.
MTOTO WA AJABU AZALIWA DODOMA MADAKTARI NA WAUGUZI WAPIGWA NA BUTWAA
BINTI AOLEWA KWA KILO MBILI TU ZA SUKARI
Mmoja wa wanafunzi walioongoza mtihani wa Taifa wa Darasa la saba mwaka huu mwenye umri wa miaka 16 anadaiwa kuozwa kwa mwanaume mwenye miaka 50 baada ya wazazi wake kupewa sukari kilo mbili kama mahari.Kutokana na hali hiyo mtandao wa kuelimisha jamii kuhusu ukeketeji Mkoani Kilimanjaro NAFGEM umefanya jitihada za kumuokoa pamoja na wanafunzi wengine15 waliotaka kufanyiwa vitendo vya ukeketaji kwa ngariba.
Subscribe to:
Posts (Atom)